Taasisi isiyo ya kiserikali inayoitwa,’Rejoice and Hope Ministries’, -RHM,
yenye makao yake makuu nchini Marekani,
kwa kushirikiana na Madaktari nchini, watatoa matibabu ya bure katika kituo cha Pentekostal Holy Mission
maeneo ya Mbezi Jijini Dar es Salaam.
Mwasisi wa Taasisisi hiyo Dk.Rejoice Ndalima amesema
kuwa, jopo la madaktari hao kutoka Marekani, watashirikiana na madaktari wa
Tanzania na wauguzi kutoa matibabu ya
macho, uvimbe pamoja na magonjwa ya kawaida ambapo watapatiwa dawa bure baada
ya kutibiwa.
Sanjari na matibabu hayo, RHM watatoa misaada kwa jamii kama vile wajane, yatima na watoto
waishio katika mazingira magumu ambapo misaada hiyo itatolewa Jumamosi hii
katika Kanisa la Pentekostal Holliness Ubungo Jijini Dar es Salaam.
Taasisi hiyo ya RHMI, hutoa misaada mara kwa mara kwa
jamii ambapo mwaka jana walikuwa Mkoani Morogoro na walifanikiwa kuwahudumia
bure wagonjwa mia tano.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni