YESU NI JIBU

Jumanne, 21 Mei 2013

UADUI MKUBWA WA UKRISTO SIO DINI NYINGINE ILA NI UKRISTO WA KIBAYOLOJIA



                             

Imeelezwa kuwa adui mkubwa wa ukristo si dini nyingine wala mamlaka za kisiasa, bali ni ukristo unaoenea kibaiolojia pasipokuwa na Roho Mtakatifu.

Hayo yameelezwa na Mwangalizi Mkuu wa Wapo Mission International, Askofu Sylivester Gamanywa wakati wa maadhimisho ya kilele cha  wiki kumi na saba za Ibada ya ujazo wa  Roho Mtakatifu iliyofanyika Jumapili iliyopita katika Ukumbi wa BCIC Mbezi Beach Jijini Dar es Salaam.

Aidha, Askofu Gamaywa amebainisha kuwa, ukristo usioambatana na Roho Mtakatifu ambaye ndiye anayefundisha, si ukristo halisi bali ni imani potofu na kwamba uzao wa kikristo hutokana na Mungu kinyume na uzao wa kibaiolojia.
Huku akishangiliwa na maelfu ya watu waliohudhuria maadhimisho hayo ambayo yameangukia Sikukuu ya Pentekoste, Askofu Gamanywa amesisitiza kwamba kama Mkristo hajaokoka, Mbinguni haingii kamwe hata kama amebatizwa.
Ameeleza kuwa, lengo la maombezi hayo ya ujazo wa Roho Mtakatifu, ni kumtambulisha Mungu katika utendaji wake wa nafsi tatu ambazo ni Baba, Mwana na Roho Mtakatifu na uzao wake wa kiroho.







Askofu Gamanywa akiwafundisha juu ya changamoto ama uadui wa dini ya kikristo






Askofu akiwaombea waumini ambao wamefika mbele ya madhabahu kwa le
ngo la kupata maombi na maombezi juu ya ujazo wa Roho Mtakatifu








Askofu akiwaongoza waumini  na kuongoza katika maombi  huku wakiinua mikono yao juu.


























Hapa maombi yamekolea uongozi wa Roho Mtakatifu ukichukua nafasi

























Mchungaji Amon Kilahiro anayepiga gitaa akiongoza
kikundi cha kusifu na kuabudu cha BCIC Mbezi beach katika ibada ya ujazo wa Roho mtakatifu.






Waimbaji wa kikundi cha kusifu na kuabudu cha BCIC wakibubujika katika ibada ya ujazo wa Roho mtakatifu.











muumini huyu akiomba kwa roho na kweli katika  ibada ya maombezi ya ujazo wa Roho mtakatifu







Waumini wakiomba ujazo wa Roho mtakatifu pamoja na kuombea mahitaji mengine mbalimbali katika ukumbi wa BCIC Mbezi beach.















































Hapa lazima kieleweke






































Hakuna maoni :

Chapisha Maoni