Mwanafunzi wa Shule ya Sekondari Keko Wilayani Temeke
Jijini Dar es Salaam, Edson John mwenye umri wa miaka kumi na tatu aliyekuwa
anasoma kidato cha pili, amekutwa amejinyonga kwa kutumia kamba ya katani
aliyoitundika kwenye mti.
Kamanda wa Polisi mkoa wa kipolisi Mkoani Temeke,
Engelbert Kiondo amedhibitisha kutokea kwa tukio hilo maeneo ya makaburini Temeke na kijana huyo
alikutwa na karatasi yenye ujumbe mfupi
kwamba ameamua kujinyonga kwa kusingiziwa maneno ya uongo.
Hata hivyo, Kamanda Kiondo alieleza kuwa, sababu za kujinyonga kwa kijana huyo bado
hazijafahamika na mwili wake umehifadhiwa Hospitali ya Wilaya Temeke kwa
uchunguzi zaidi.
Suala la watu kujinyonga katika jiji la Dar es saalam
linaendelea kushika kasi kwani kila kukicha hutolewa taarifa za watu kujinga
ama kujaribu kujiua hivyo ni nyema hatua na njia maususi zichukuliwe ili
kudhibiti na kuondoa tatizo hilo.
Imeonekana kuwa shetani anasababisha watu kujiua kwa
kusingizia vitu mbalimbali kama kuachwa na wapenzi wao wengine magonjwa,shida,kukataliwa
jambo ambalo ukichunguza kwa undani sio la kweli ni hila za adui kuwaangamiza
wanadamu bila kufikilia toba.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni