YESU NI JIBU

Jumatano, 17 Januari 2018

BROFOA HUTOA ELIMU BORA KUWASAIDIA WALIOKATA TAMAA NA KUSHINDWA KUENDELEA NA ELIMU

Mkurugenzi wa Brothers Academy Ndugu Robart Rwezaura akizungumza jambo na waandishi wa habari.
 Na Stelius Sane,
Imebaishwa kuwa elimu ambayo hutolewa katika mfumo usio rasmi imekuwa msaada mkubwa sana Kwa wale ambao walishindwa kupata elimu katika mfumo rasmi kutokana Na matatizo mbalimbali ya kifamilia ama sababu zingine.
Kauli hiyo imetolewa Na mkurugenzi wa brothers font of academy ndugu Robart Rwezaura wakati akizungumza Na gazeti hili ambapo alisema kuwa mfumo usio rasmi umekuwa mkombozi wa kielimu Kwa wale watu walioshindwa kusoma Katika mfumo rasmi.

Aidha aliongeza kuwa kuna baadhi wa watu hasa watoto wa kike ambao walishindwa kufikia malengo yao kutokana na ujauzito Kwa kurubuniwa au kubakwa Na kupata ujauzito hali iyoua ndoto yao ya kielimu.
AlifafAnua kuwa endapo ulishindwa kupata elimu katika mfumo rasmi usisite kupambana kutafuta elimu maana serikali imepitisha na kuruhusu elimu kutolewa katika mfumo huo kwa mujibu wa sheria za nchi.
Akifafanua kwa undani alisema kuwa Brother academy umejikita kuwasaidia wale ambao hawakupata elimu Kwa mfumo rasmi,hivyo hutoa elimu ya sekondari Kwa miaka miwili Yaani Qulify test QT na elimu kidato cha tano Na sita Kwa mwaka mmoja sambamba Na Kwa wale wanaorudia mtihani wa kidato cha nne Na sita Yaani Resetters.
Pamoja Na hayo wamejikita kutoa elimu ya computer programu zote,lugha ya kiingereza na kifaransa kutokana na uhitaji ulipo ndani ya jamii Na wapo mbioni kuanzisha Mafunzo ya kichina.
Ndugu Rwezaura alifafanua kuwa kila mmoja anaweza kupata elimu pale atakapoamua kusoma hasa pale Brothers maana wao huwapokea watu waliofanya vibaya katika mitihani Yao ya mwisho na Na pia Kwa wale ambao hawakufanikiwa kusoma ama kupata elimu kutokana na changamoto mbalimbali za kimaisha.
Baada ya kuona uhitaji huo Brothers kama taasisi wamewatafuta walimu wenye taaluma ya ualimu na walifuzu katika vyuo vikuu wenye mzigo na nia ya kuwasaidia wale walioshindwa kupata elimu katika mfumo rasmi pamoja Na waliofanya vibaya katika mitihani yao ya mwisho wa kidato cha nne na sita Na kupelekea kukata tamaa ya kupata elimu na ndoto zao kielimu kufa.
Aliendelea na kusema Brothers academy imekuwa ikifanya vizuri katika mitihani ya QT na ya kidato cha Sita Kwa mwaka mmoja katika shule zinazotoa elimu katika mfumo usio rasmi Hali inayosababisha kuona ndoto ya baadhi ya watu kielimu kuanza kufufuka.
"Mpaka sasatnaendelea kufanya vizuri hali inayosababisha kuona ndoto za watu kuanza kufufuka maana mpaka Sasa tuna baadhi ya walimu ambao wameshapata shahada yao ya ualimu kutoka vyuo vikuu ambao walipitia ama walipata elimu Kwa mfumo usio rasmi hapa Brothers academy Na Sasa Ni walimu na baadhi wanafundisha hapa"alisema Rwezaura.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni