Kumtumikia Mungu kwa uaminifu yeye atakuinua kwa wakati wake
usipozimia roho maana hutenda zaidi ya akili za wanadamu.
Hii ni baada ya mwimbaji wa nyimbo za injili Tanzania Zakaria
Kenyata kutambulisha rasmi albamu yake ya watakuheshimu kesho katika uwanja wa
kimataifa nchini China.
Aidha Ndugu Zakaria Kenyatta ameandika kwenye ukurasa wake wa
facebook kuwa "Unaweza ukasota zaidi ya miaka 30 kwenye Huduma hakuna hata
anae sema hodi hapa lakini Mungu anaweza kukutambulisha dakika moja tu ukasahau
kusota kote kwa miaka hiyo usikate tamaa new album ya watakuheshimu kesho ya
tambulisha katika uwanja wa kimataifa Leo China.
Mwimbaji Zakaria Kenyatta akitambulisha albamu yake ya watakuheshimu Kesho katika uwanja wa kimataifa wa China.
Watu wa Taifa la China waliofika katika uwanja wa kimataifa kushuhudia utambulisho wa albamu ya mwimbaji wa kitanzania Zakaria Kenyatta.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni