YESU NI JIBU

Jumamosi, 3 Machi 2018

KUKOMBOA WAKATI SIO KWENDA NA WAKATI:


Na Stelius Sane,
Imebainika kuwa kila mmoja akikomboa wakati badala ya kwenda na wakati atafanikiwa katika maisha yake kiuchumi,kiafya,kisiasa na hata kiroho kutokana na kuwa katika wakati sahihi wa kile anachokifanya.

Hayo yalisemwa na mchungaji Bernard Jomalema wa huduma ya wapo mission International wakati akizungumza na gazeti hili jijini Dar es salaam ambapo alisema kuwa kuna tofauti ya kukomboa wakati na kwenda na wakati ila asilimia kubwa ya watanzania hawajatofautisha na ndiyo maana kuna malalamiko na manung'uniko ndani ya jamii.
Mchungaji Jomalema alisema kuwa kila mmoja akikomnboa wakati malalamiko katika sehemu za ibada,sehemu za kazi na hata katika familia itapungua kama sio kwisha kabisa maana kila mmoja atafahamu anatakiwa kufanya nini na kwa wakati gani.
Aidha aliongeza kuwa ili Mungu amwinue mwanadamu katika maisha yake ni pale tu atakapokomboa wakati maana kuna baadhi ya watu ama waumini pamoja na wananchi wanalalamika ila bado wao wenyewe wanasababisha maisha kuwa magumu.
kukomboa wakati ni pale ambapo unafanya kinachotakiwa kwa wakati sashihi na kwa muda muafaka na sio kuwa unawasili sehemu ya majukumu na kuanza kufanya majukumu mengine kinyume na yale yanayohitajika kufanya kwa muda ule ulipo.
Ni kweli kuna mambo hayaendi ila sio kwamba sababu ni Mungu ama shetani ila ni wewe mwenyewe umekuwa kikwazo cha mafanikio ya maisha yako sasa ni wakati wa kufunguliwa ili utambue yale ambayo Mungu anataka ufanye

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni