YESU NI JIBU

Jumanne, 20 Februari 2018

WAUMINI WASHAURIWA KUHUBIRI JUU YA UFALME WA MUNGU:


Askofu mkuu wa kanisa la Faith Community Pentecoste Church (FCPC) lililopo Mbezi Maramba mawili jijini Dar es salaam,Barthelomeo Sheggah amewataka wakristo kuhibiri juu ya ufalme wa mbinguni ikiwa ni njia pekee ya kulijenga kanisa la Mungu kulingana na misingi ambayo Yesu alituwekea tangu mwanzo 

Akizungumza katika Ibada wiki iliyopita Askofu Sheggah ameuelezea kuwa ufalme huo ni katika ulimwengu ambao hauonekani kwa macho ya kawaida bali kanuni zake zipo na zinafundishika 


Askofu Sheggah alisema watu wanapaswa sana kufahamu kanuni za ufalme huo ambapo ili kila mmoja aweze kuzitenda kanuni hizo anahitaji hekima kutoka kwa Mungu.

Alisema kanisa limepoteza ufalme na inatupasa kuurudisha ambapo aliitaja njia moja wapo ni kutubu

"Yesu alianza kuhubiri juu ya ufalme wa mbinguni umekaribia lakini pia Yohana nae alihubiri vivyo hivyo tangu mwanzo ambapo aliwataka watu kutubu" alisema Askofu Sheggah.

Aidha alithibitisha maneno hayo katika vitabu mbalimbali kwenye Biblia na kutolea ufafanuzi juu ya neno 'Umekaribia' kuwa lilimaanisha wakati umefika au upo sasa ambapo akautambua uelewa huo kuwa ni wa kimapinduzi.

Askofu Shaggah aliongeza kuwa sasa imefika wakati hata serikali haiwezi kuomba msaada kwa viongozi wa dini  kutatua baadhi ya mambo kutokana na kanisa kupoteza ufalme.

"inatupasa na ni muhimu kuwa na ufalme kwani hata zamani viongozi wa nchi walipofika wakati wanashindwa kutatua mambo waliwatafuta viongozi wa dini  lakini kwetu hakuna na hilo linachagizwa na kuupoteza ufalme"alisema 

''Ipo haja ya kubadilika katika mwaka huo na kuanza kutafuta namna ya kuurudisha ufalme kwa kuhubiri sana ingawa mengine ni muhimu lakini hili la ufalme litarahisisha mengine yote"aliongeza Askofu Sheggah.

Alitolea mfano Yesu alikemea pepo kwa kuwawekea mikono wenye pepo nao pepo wakatii na kutoka lakini sasa Wachungaji, Manabii na hata Mitume wanakemea hata saa matatu pepo bado hatoki, hii ni kwa sababu tumekosa ile nguvu ya kifalme.

"Tukiwa na ufalme kila kitu kitakuwa rahisi maana nguvu ya ufalme huo hakuna wa kuufananisha nao kwani tunakuwa tumebeba mamlaka ya kimungu" Alimalizia.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni