YESU NI JIBU

Jumatano, 7 Februari 2018

WATUMISHI WA MUNGU WATAKIWA KUKOMBOA WAKATI KATIKA HUDUMA ZAO:

 Askofu na mchungaji bernad Jomalema wa BCIC  kutoka kushoto akiwa na askofu Selestine Kato wa kanisa la Blessing Community wakifuatilia mafundisho ambayo yalikuwa yakifundishwa na mwali Mtito wa ICM.

 Askofu na mchungaji Kiongozi Selestine Kato akifundisha watumishi wa Blessing Community kwenye Kongamano liloandaliwa na kanisa hilo kwa lengo la kuwanoa watumishi wake
 Mtangazaji wa Wapo Radio na mwandishi wa gazeti Msemakweli pia mmiliki wa Blog hii akifundisha umuhimu wa watumishi wa Mungu kutumia vyombo vya habari na mawasiliano kwa ujumla.
 Merrystela Kato katikati akiwa na baadhi ya watumishi katika kongamano la watchungaji na watendakazi wa kanisa la Blessing Community wakiwa katika ibada ya kusifu na kuabudu.
 Mwalimu Menrald Mtitu  Kutoka ICM akiwafundisha wachungaji na watumishi waliohudhuria kwenye Kongamano huko Mpera Kisemvule.
Ni wakati wa kumwabudu Mungu katika Roho na kweli ndiyo alivyonekana askofu Kato akifanya kwenye kongamano la wachungaji na watumishi wa kanisa la Blessing Community
Na Stelius Sane,
Imebainishwa kuwa mwamini yeyote anapokomboa wakati anafanikiwa kufikia viwango vya juu kiroho na kimwili hali ambayo itasaidia hata wanaomzunguka kuwa na furaha ya kumtafuta na kumtumikia Mungu.
Hayo yamebainishwa hivi karibuni na mchungaji Bernad Jomalema wakati akiwafundisha baadhi ya wachungaji na watendakazi wa kanisa la Blessing Community  iliyopo chini ya askofu Selestine Kato waliokuwa kwenye kongamano la kujifunza masuala mbalimbali ya kihuduma na kijamii pia.
Aidha Askofu na mchungaji Jomalema alisema kuwa kumtumikia Mungu si mateso na sio mzigo mzito kama wengine wanavyowaza ila ni kazi nyepesi sana kama umeitwa kweli na MUNGU Kumtumikia na sio hisia zako zinakusukuma,kama ni hivyo utaona kumtumikia Mungu ni mzigo tena mzito sana.
“Leo ninyi watumishi na viongozi mmekusanyika hapa lengo sio kwamba hamfahamu kutumika hapana ni kuinuana na kutiana moyo katika utumishi wenu mlioitiwa na Mungu katika maeeneo yenu ya huduma,hivyo ni vyema kila mmoja kusimama katika nafasi yake kama yeye kumtumikia MUNGU wake kwa bidii,”alisema mchungaji Jomalema.
Kwa upande wa askofu kiongozi wa kanisa hilo la Blessing Commuty askofu Kato alisema kuwa yeye anafurahishwa sana opaleanapoona watu wakimtumikia Mungu kwa bidii katika maisha yao na kumzalia matunda yatakayodumu.
Askofu Kato alisema kuwa kwa sasa wanampango wa kuwafikikia wale ambao hawajafikiwa na injili ya Yesu Kristo katika maisha yao nao watafunguliwa na kuwa salama maana kuna watu wengi wamefungwa katika maisha yao na vifungo mbalimbali vya magonjwa,mapepo na hata rohonza umaskini imewaklia kiasi kwamba kila wanalolifanya hawafanikiwi sasa inabidi kuwafikia ili Bwana Yesu awafungue na kuwaweka huru mbali na mateso na dhambi.
“Kwa sasa tunamshukuru Mungu maana tunawafikia baadhi ya watu hasa katika maeneo ya Malela tunamuona Mungu akiwahudumia na kuwainua waliofungwa kwa viwango vya juu sana,”alisema Askofu Kato.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni