YESU NI JIBU

Jumatano, 21 Februari 2018

KULINDA MOYO NI KUPONYA ROHO NA MWILI:


Imebainishwa kuwa kulinda moyo ni ia mojawapo ya kuepukana na magonjwa yanayoweza kushambulia mwili sanjari ya kuepukana na vifo vinavyotokana na magonjwa ya moyo.
akifundisha somo la namna ya kulinda moyo na Bi Monica lawrent ambaye yupo chini ya huduma  ya mwana wa Adamu alikuja kutafuta na kuokoa kilichopetea  inayongozwa na mtumishi Saimon Jonath iliyopo mkoani Morogoro ambapo amesema kuwa ili kuepukana na magonywa yanayoshambulia moyo na kuonekana katika mwili na roho ni kulinda moyo kama biblia inavyosema.

Akinukuu kitabu cha Mithali 4:23 amcha kimeandikwa kuwa linda moyo wako kuliko yote uyalindayo;maana ndiko zitokako chemchemi za uzima,
Aidha Bi Monica alielezea maana ya Moyo na  kazi yake na unahusikaje?  na uzima wako wa roho na mwili? ambapo alianza kwa kusema Moyo ni kiunganishi cha roho na mwili.
"Haujui kuwa moyo unaposhindwa kufanya kazi roho haiwezi kuishi ndani ya mwili tena? Yaani mauti humkuta mtu huyo na matokeo ya moyo yanaweza kuleta madhara ktk roho yako, kama mithali15:13b inavyoelezea kuwa bali kwa huzuni ya moyo roho upondeke."Alisema Bi Monica.
Aliongeza kuwa mtu mwenye moyo wa namna hii roho yake haiwezi kuwa na nguvu hata ya kuomba, pia matokeo yake huleta madhala ktk mwili,sawa na kitabu cha mithali 14:30 ilivyoandikwa kuwa moyo ulio mzima ni uhai wa mwili; bali husuda ni ubovu wa mifupa.
Mtu anapokuwa na matatizo ya moyo humpelekea kuwa mgonjwa wa mwili hata kulazwa, na hii huonekana dhahiri kwa mtu mwenye presha.
Hata hivyo aliongeza kuwa jambo ambalo unaliwaza ktk moyo ndiyo linaloleta matokeo ktk mwili au ktk roho yako,kama mithali 6:18 inavyoelezea moyo uwazao mawazo mabaya;miguu iliyo myepesi kukimbilia maovu;
"Sasa tunapata kuona kuwa nikwanini tuliambiwa tulinde sana moyo kuliko hata mwili,ni kuhakikisha moyo wako uko salama wakati wote,kutengeneza moyo si kazi ya MUNGU wala sio ya jirani yako bali inakuhusu wewe",alisema Bi Monica.
Hivyo aliendelea kuwa kusema kuwa  mwenyewe,ukiuandaa moyo ktk kusamehe ni wewe mwenyewe  hata kama utakuwa umekosewa kosa kubwa kiasi gani,hautàlibeba moyoni bali utaliachilia.
Akinukuu kitabu cha  mithali 16:1a alisema kuwa maandalio ya moyo ni ya mwanadamu; jitahidi kuuandaa vyema moyo wako ili kupata majibu bora ktk mwili na ktk roho.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni