YESU NI JIBU

Jumatano, 18 Julai 2012

WAJANE WATAKIWA KUFUNGUKA KIROHO KUJIAMINI NA KUTOJIDHARAU


Wito umetolewa kwa wanawake wajane nchini, kufunguka kiroho, kujiamini na kutojidharau ili waweze kujijengea uwezo wa kiuchumi kupitia ujasiriamali na kulea vyema watoto wao.
Hayo yameelezwa na Mwenyekiti wa Huduma ya Elishadai inayosimamia wanawake wajane, Mwinjilisti Agusta Ernest Kitea kutoka Kanisa la Gosheni lililopo maeneo ya Ilala Mchikichini wakati akizungumza kwenye Kongamano la siku moja la wanawake wajane lililofanyika katika Ukumbi wa Parokia ya Msimbazi Jijini Dar es Salaam.
Mwinjilisti Agusta ambaye alifiwa na mumewe miaka saba iliyopita huku akimwachia mtoto mchanga amebainisha kuwa, huduma yake inakabiliwa na changamoto kadhaa ikiwemo ukosefu wa fedha.
Kongamano hilo la pili kufanyika nchini, limehudhuriwa na takribani wanawake 180  ambapo kongamano la kwanza lilifanyika Julai 16 mwaka jana katika Ukumbi huo na kongamano lingine linatarajiwa kufanyika Desemba 18 mwaka huu.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni