YESU NI JIBU

Jumatano, 18 Julai 2012

KIBURI NI MBAYA KATIKA MAISHA YA MWAMINI ALISEMA ASKOFU SYLVERSTER GAMANYWA


Kuwa na kiburi kutokana naulichonacho imeelezwa kuwa ni mojawapo ya njia zinazobasabaisha mwaminini asiweze kupokea Baraka zake kutoka kwa Mungu kwani kiburi kinamfanya mwamini kujiona kuwa bora kuliko mwingine.
Kauli hiyo  ilitolewa hivi karibuni na askofu mkuu wa WAPO Mission international askofu Silvester Gamanya wakati akifundisha juu ya somo la kiburi kwenye mchesha uliofanyika katika ukumbi wa BCIC Mbezi beach jijini Dar se saalam.
Kiburi ni tatizo kubwa linalowakabili waumini wengi kwenye madhehebu yao na dini zao na suala hilo linasababisha uwepo wa Mungu kuwa na mipaka ndani ya waumini,ni vyema kila mwamini kwa nafasi yake kukataa na kupinga kwa juhudi zote juu ya tatizo hilo la kiburi lisiwepo ndani ya maisha yake.
Mwanadamu anaweza kuwa na kiburi ya mali ,elimu aliyonayo ama fedha na inasababisha mwanadamu huyo kujiona kuwa hakuna kinachoweza kumkwamisha ama kumzuia katika maisha yake kufanya jambo ambalo kwa ukweli ni kujidanganya katika maisha yake.
Alisema kuwa na elimu fedha na utajiri wa kila aina ni vizuri kila mwanini ama mwanadamu asiwe na kiburi maana ni mbaya sana  kiasi kwamba inasababisha hata pamoja na kuwa na vitu hivyo kuonekana kuwa haufai mbele za Mungu na mbele za wanadamu.
Mkesha huo ni mfululizo ya mikesha ya urejesho ambayo hufanyika kila mwisho wa mwenzi katika vituo vya BCIC Mbezi beach na BCIC temeke na huwa maombi na maombezi hufanyika kwa wale wenye shida na matatizo mbalimbali katika maisha yao na watu wengi hufunguliwa.
Kutokana na hayo askofu amekuwa akifundisha kwa umakini na ufasaha zaidi juu mafundishao yanayohusu maisha ya wanadamu pamoja na kuwepo kwa malalamiko ya waumini kulalamikia hali ngumu ya maisha basi njia pekee ya kupata ufumbuzi ni kumwamini bwana Yesu.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni