Imeelezwa
kuwa ni vyema wanadamu kumnyenyekea Mungu katika maisha yao ya kila siku ili
waweze kuishi maisha ya amani na usalama katika maisha yao sambamba na kuifuata
njia za kweli.
Akizungumza
katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya kanisa la EAGT Saranga
jijini Dar es salaamu mchungaji Florian Katunzi amesema kuwa imetosha kwa
mwanadamu kutenda dhambi katika maisha yake kwani tangu mwanadamu kuanza
kutenda dhambi hajawahi kutosheka katika maisha ya dhambi
Aidha
mchungaji katunzi amesema kuwa haijalishi kuwa unafanya kazi ya namna gani kama
hujaokoka ni kazi bure maana wapo wengine wanaitwa wafia dini kwani wanakuwa
walevi na bado wanakwenda makanisani na wakati mwingine anakwenda kwa waganga
na wachawi huku akisema wanamwabudu Mungu huku maisha yake hayampendezi Mungu.
Pamoja na
hayo aliongeza kusema kuwa ni vyema kumtafuta yesu katika maisha yako na katika
makusanyiko mbalimbali kumekuwepo watu ambao wanakuwa kama ni wasindikizaji katika maisha
ya dini na kuendelea kujificha kwa kivuli ya dini na kuendelea kutenda makosa
na dhambi.
Hata hivyo
mch.Katunzi amesema kuwa wapo wengine wamekuwa wakifuga majini katika nyumba
zao badala ya kufuga mifugo na wanyama wengine wa kufugwa badala yake wanafuga
majini kwa lengo la kuwatesa wanadamu wengine .
“Bila Yesu
mwanadamu huwezi ukakwepa majini na wachawi sambamba na wachawi bila kumpokea bwana Yesu kama bwana na
mwokozi wa maisha yako bila hivyo utaendelea kuteseka katika maisha yako ya
kawaida kama wanadamu wengine hivyo ni vyema umkubali Yesu katika maisha yako”
alisema mchungaji Katunzi.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni