Wakazi wa Zanzibar na Jamii kwa ujumla, wamehimizwa
kujitokeza kwa wingi kuhudhuria semina ya ujasiriamali ya siku tatu inayoanza
kesho hadi Julai19 mwaka huu.
Akizungumza na Wapo Radio Fm,
Mkurugenzi wa Kampuni ya Ujasiriamali ya I C B Jijini Dar
es Salaam, Mchungaji Israel Ernest wa Huduma ya 'Uamsho Kivule',
ameeleza kwamba semina hiyo itafanyika Visiwani
Zanzibar katika Uwanja wa CCM Kiembesamaki.
Kwa mujibu wa Mchungaji Israel, kufanyika kwa semina hiyo kunafuatia
maombi ya muda mrefu wa wakazi wa Zanzibar
ya kufundishwa masuala ya ujasiriamali ili wajikomboe kiuchumi na kuondokana na
umaskini.
Ameongeza kuwa, bidhaa
zitakazofundishwa kinadharia na vitendo wakati wa semina hiyo ni pamoja na utotoaji wa vifaranga, mafuta ya mgando, chaki, mishumaa, kilimo cha
uyoga na keki za harusi.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni