YESU NI JIBU

Jumatano, 18 Julai 2012

MAFUNDISHO YA UJASIRIAMALI YATOLEWA KWA SIKU TATU KIVULE


Wakazi wa Zanzibar na Jamii kwa ujumla, wamehimizwa kujitokeza kwa wingi kuhudhuria semina ya ujasiriamali ya siku tatu inayoanza kesho hadi  Julai19 mwaka huu.

Akizungumza na Wapo Radio Fm, Mkurugenzi wa Kampuni ya Ujasiriamali ya I C B Jijini Dar es Salaam, Mchungaji Israel Ernest wa Huduma ya 'Uamsho Kivule', ameeleza kwamba semina hiyo itafanyika Visiwani  Zanzibar katika Uwanja wa CCM Kiembesamaki.

Kwa mujibu wa Mchungaji Israel, kufanyika kwa semina hiyo kunafuatia maombi ya muda mrefu wa wakazi wa Zanzibar ya kufundishwa masuala ya ujasiriamali ili wajikomboe kiuchumi na kuondokana na umaskini.

Ameongeza kuwa, bidhaa zitakazofundishwa kinadharia na vitendo wakati wa semina hiyo ni pamoja na  utotoaji wa vifaranga,  mafuta ya mgando, chaki, mishumaa, kilimo cha uyoga na keki za harusi.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni