YESU NI JIBU

Jumapili, 22 Julai 2012

Aliyekuwa mtangazaji wa kipindi cha michezo Joseph Mapunda anatazikwa katika makaburi ya chang'ombe jijini Dar es salaam.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi mdogo wake marehemu bwana ZICO MAPUNDA amesema kuwa mwili wa marehemu utaagwa nyumbani kwake mtoni kijichi na kupelekwa kwenye makaburi ya chang'ombe kuzikwa.

Marehemu amemwacha mjane na watoto wawili wa kiume ambapo kwa mujibu wa ndugu huyo amesema kuwa marehemu alikuwa akisumbuliwa na tatizo la tumbo ambalo alilazwa katika hospitali ya wilaya ya Temeke.
Marehemu amelazwa katika hospitalini hapo kwa muda wa siku mbili na siku ya tatu akapoteza maisha hospitalini hapo

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni