Mwandishi wa kitabu kipya cha
utafiti kwa lugha ya Kiswahili kwa elimu ya juu, Mchungaji Dk. Elia Shabani
Mligo, amekitambulisha rasmi kitabu hicho kiitwacho, 'Jifunze utafiti'.
Akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam,
Mchungaji Elia amesema kuwa, lengo la kuandika kitabu hicho kwa lugha ya
Kiswahili ni kuwarahisishia wanafunzi kufanya vizuri katika somo la
utafiti kwani wengi wao wana uelewa
mdogo wa lugha ya kiingereza.
Aidha Mchungaji Elia amebainisha
kuwa, uwezo mdogo wa wanafunzi kujieleza kupitia lugha ya kigeni, umekuwa
ukisababisha kufanya vibaya katika somo hilo
kwa wanafunzi wa elimu ya juu.
Kwa mujibu wa Mchungaji Dk.Elia, kitabu hicho kimechapishwa na Mkurugenzi wa
Kampuni ya uchapishaji Vitabu ya Jijini Dar es Salaam, Bw.Mkumbo Mtula.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni