YESU NI JIBU

Jumanne, 10 Julai 2012

MCHUNGAJI KUTAMBULISHA KITABU CHA UTAFITI ILIYOANDIKWA KWA LUGHA YA KISWAHILI





Mwandishi wa kitabu kipya cha utafiti kwa lugha ya Kiswahili kwa elimu ya juu, Mchungaji Dk. Elia Shabani Mligo, amekitambulisha rasmi kitabu hicho kiitwacho, 'Jifunze utafiti'.

Akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam, Mchungaji Elia amesema kuwa, lengo la kuandika kitabu hicho kwa lugha ya Kiswahili ni kuwarahisishia wanafunzi kufanya vizuri katika somo la utafiti  kwani wengi wao wana uelewa mdogo wa lugha ya kiingereza.

Aidha Mchungaji Elia amebainisha kuwa, uwezo mdogo wa wanafunzi kujieleza kupitia lugha ya kigeni, umekuwa ukisababisha kufanya vibaya katika somo hilo kwa wanafunzi wa elimu ya juu.

Kwa mujibu wa   Mchungaji Dk.Elia,  kitabu hicho kimechapishwa na Mkurugenzi wa Kampuni ya uchapishaji Vitabu ya Jijini Dar es Salaam, Bw.Mkumbo Mtula.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni