YESU NI JIBU

Ijumaa, 10 Juni 2016

WAUMINI WENGI WAFUNGULIWA KATIKA KONGAMANO LA SIKU 90 NDANI YA KANISA LA EAGT CITY CENTER KWA MCHUNGAJI KATUNZI


 mchungaji Katunzi akionesha kufuli ambayo ametapika mtu mmoja ambye amefahamuika kwa jina moja la Faith Ibadani baada ya kumalizika kwa maombi na maombezi.

 Mchungaji Florian katunzi akiwa na kijana aliyekuwa mwizi na kunusurika kuuwawa zaidi ya mara tatu na mtoto Husna ambaye alikuwa akianguka kila akienda shuleni na sasa amefunguliwa yupo huru.
 mchungaji Katunzi akiwa na kijana Idrisa ambaye alikuwa mwizi na kufika kanisani alifunguliwa na kuwekwa huru na sasa ni mzima anendelea vizuri.
 Ni nyama ambaye ametapika mmoja wa watui walofika kanisani hapo kutafuta msaada baada ya kuteseka kwa muda mrefu bila mafanikio na sasa amefunguliwa yupo huru
Umati wa waumini waliohudhuria ibada ya maombi na maombezi kipengele cha uweza na nguvu.
 waumini wakifurahia neno la Mungu kanisani EAGT City Center wakati mchungaji Katunzi hayupo pichani akifundisha somo la maombi na maombezi kipengele cha uweza na nguvu.
Waumini wakishangilia kwenye ibada ya neno la Mungu ndani ya kanisa la EAGT City Center,
Hali imeelezwa kuwa ya tofauti sana pale watu mbalimbali wa dini na madhehebu mbalimbali kufika katika kanisa la EAGT City Center na kufunguliwa na kuwekwa HURU mbali na magonjwa .
Hayo yamesemwa na mchungaji kiongozi wa kanisa hilo mchungaji Florian Katunzi wakati akifundisha somo la Maombi ndani mwa maombi kipengele cha Uweza na nguvu ambapo alinukuu kitabu cha Isaya 40:27-31 ambayo inasema Mbona unasema, Ee Yakobo, mbona unanena, Ee Israeli, Njia yangu imefichwa, Bwana asiione, na hukumu yangu imempita Mungu wangu asiiangalie?  Je! Wewe hukujua? Hukusikia? Yeye Mungu wa milele, Bwana, Muumba miisho ya dunia, hazimii, wala hachoki; akili zake hazichunguziki. Huwapa nguvu wazimiao, humwongezea nguvu yeye asiyekuwa na uwezo.  Hata vijana watazimia na kuchoka, na wanaume vijana wataanguka; bali wao wamngojeao Bwana watapata nguvu mpya; watapanda juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia.
Aidha amesema kuwa lengo la siku hizi 90 ni kuwafikia watu wengi wa dini mbalimbali na madhehebu mbalimbali ili waweze kufunguliwa.
"Ila upinzani unainuka kwa njia nyingi ili usihudhurie ibada ya siku 90 ila unawezuiliwa na dini sasa imefika wakati wa kuvuka mipaka ya dini dhehebu ili uwekwe huru'alisema mchungaji Katunzi.
Aliongeza kuwa  akili za Mungu hazichunguziki maana anampa nguvu na uwezo wewe usiye na nguvu wala uwezo maana Mungu ni mwenye uwezo na anaweza kuzipindua nguvu za giza , wachawi na waganga ili watu wa Mungu wainuliwe na uzao wa mwanamke usiendelee kuteseka na kutaabika.
 Alinukuu kitabu cha Yoshua 6:1 na kusema kuwa Basi Yeriko ulikuwa umefungwa kabisa kwa sababu ya wana wa Israeli; hapana mtu aliyetoka wala hapana mtu aliyeingia. 
"Uzao wako unaweza kufungwa ili kisiwepo kinachoingia wala kutoka maana kila kizuizi kilichowekwa kinaondoshwa kwa jina la Yesu",aliongeza mchungaji katunzi.
Alisema kuwa kitabu cha Yoshua 5:13-14 kinasema, Lazima ufahamu kuwa kuna adui wanaokuzunguka na wanatafuta njia ya kukuangamiza wa kusimama mbele zako maana Mungu wako yupo ambaye anaenda kukuokoa na kukuweka huru.
Uwezo wa kumiliki na kutawala katika ulimwengu wa roho na mwili uko ndani yetu maana Uwezo huu u juu ya ufalme wote na mamlaka,tangu mwanzo wa mwanadamu Mungu alimpa uwezo na nguvu za kiutawala ambapo maandiko yanasema; katika Mwanzo 1:21-28“Mungu akasema, na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi. Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba,
Hata hivyo Mungu aliweka nguvu ya kutawala ndani ya mwanaume na mwanamke ambapo kuna funguo kumi na saba za kufungua njia hivyo njia iliyofungwa lazima ifunguliwe.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni