YESU NI JIBU

Ijumaa, 3 Juni 2016

MWIMBAJI WA NYIMBO ZA INJILI LILIAN NAMAN NGOWI AJIPANGA KUWAFIKISHIA WENGI INJILI KWA NJIA YA UIMBAJI



Mwimbaji wa nyimbo za injili Liliana Naman Ngowi akiwa na kwaya uinjilisti Kijitonyama walipofanya Michigan Marekani.
Lilian ni wa pili kutoka kushoto





 Akiwe sehemu ya kuchukulia video
 Mwimbaji Liliana Naman Ngowi akirekodi akiwa studioni kurekodi nyiz za albamu yake ya
Mwimbaji wa nyimbo za Injili Liliana Naman Ngowi amesema kuwa amejipanga kupeleka injili kwa wengi kwa njia ya uimbaji katika sehemu mbalimbali ndani na nje ya Taifa la Tanzania.
Alisema hayo wakati akizungumza na blog hii ambapo aliweka bayana mikakati yake ya kuwafikia wengi kwa njia ya uimbaji,ili kuwafikia hasa wale watu wa vijijini.
Aidha alisema kuwa huduma ya uimbaji alianza toka akiwa mdogo katika shule ya jumapili maana wazazi wake walikuwa ni wakristo hivyo walimlea katika njia ya kikristo hadi hapo alipokuwa mtu mzima na sasa ni mwimbaji binafsi.
"Mimi toka mwanzo  nilikuwa napenda kuimba na nimeshirikiana na wenzangu toka shule ya msingi hadi sekondari nimekuwa nikiwaongoza wenzangu katika kuimba katika jumuiya ya wanafunzi  UKWATA,na nimeshaimba na vikundi mbalimbali kama vile KKKT ,kijitonyama kwaya ya uinjilisti kwa zaidi ya miaka 14,nimeimba kwenye mass kwaya yenye waimbaji mia mbili",alisema Lilian.
Aliongeza kuwa amekuwa na uzoefu katika kuimba kwani pia ameshirikiana na kikundi cha kusifu cha kijitonyama na cha Anzania Front na pia alishiriki katika semina na huduma mbalimbali na wengi walifunguliwa kwa njia ya uimbaji.
Mbali na kushiriki katika uimbaji wa Injili alisema kuwa alishirikiana na Tm Music na walipata fursa ya kuhudhuria mkutano wa kupambana na kuzuia Rushwa ,na hadi sasa albamu yake yenye nyimbo tisa imekamilika katika mfumo wa CD na DVD.


Liliana Naman Ngowi mbali na kuwa mwimbaji wa nyimbo za injili bado ni mjasiriamali na sasa anenda kuzindua albamu yake tarehe  19 June  2016 katika kanisa la KKK Kinyerezi kuanzia saa nane mchana na kuendelea na hakuna kiingilio,na waimbaji mbalimbali watamsindikiza Lilian Naman Ngowi katika uzinduzi wa Albamu yake ya Tumaini limerudi.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni