MWINJILISTI DAUDI MASHIMO AKIZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI HAWAPO PICHANI KATIKA UKUMBI WA HABARI MAELEZO JIJINI DAR ES SALAAM,
Mwinjilisti wa Kanisa la Calvary ministry lilopo Mwenge Mlalakuwa jijini Dar es Salaam Daudi Mashimo amewataka watumishi wanaojiita manabii kujitokeza kuomba msamaha kwa Watanzania ndani ya siku 14 kwa kudanganya kuwa wao ni manabii.
Amesema kuwa kwa sasa Tanzania kuna mlipuko mkubwa wa Manabii wa uongo hivyo waache kujiita manabii na wajitokeze kuomba msamaha kwa Mungu na kwa taifa kwa ujumla kwani wote ni matapeli wa kiroho.
Amesema kuwa kwa sasa Tanzania kuna mlipuko mkubwa wa Manabii wa uongo hivyo waache kujiita manabii na wajitokeze kuomba msamaha kwa Mungu na kwa taifa kwa ujumla kwani wote ni matapeli wa kiroho.
“Nabii ana sababu ya kuwepo na pia hana dini hivyo Mungu mwenyewe ndiye
anaempa ujumbe kuja kutoa kwa wahusika na hao wanaojiita manabii hawana
sifa ya kuwa manabii bali ni wapigaji kwani huduma wanazozifanya si za kinabii”
alisema Mashimo.
Ameongeza kuwa kwa sasa nchi yetu imegubikwa na mambo mengi sana hivyo kama
nabii anapaswa kufahamu mambo hayo kwa ajili ya kusimama ili kuponya taifa kwa
kutahadharisha katika mambo mbalimbali ambayo yanatarajia kutokea.
“Nabii anajulikana kwa matendo yake hivyo wanaojiita manabii ni matapeli
wa kiroho hakuna wa kweli hata mmoja hivyo wanapaswa kutubu mbele za
Mungu na kuacha mara moja kujiita kuwa wao ni manabii” alisema Mwinjilisti
huyo.
Amewataja nabii ambao si wa kweli kuwa ni pamoja na nabii Joe David
wa Ngurumo ya upako la Arusha, Mkombo wa Boko Magengeni, Mtume na Nabii
kimbilio wa segerea, Malisa wa Mwanza, Milili wa kinondoni
Studio na wengine wote wanojiita nabii na kusisitiza kuwa waache mara
moja kujiita nabii.
Mbali na hayo watanzania wanapaswa kuwa makini na kuepukana na manabii wa
uongo ili kukomboa taifa kwa ujumla.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni