Askofu Geofrey Masawe askofu wa jimbo la Mashariki Kasakazini na pia ni mchungaji kiongozi wa kanisa la TAG Sahara Spiritual Center
Mwinjisti Kambona Mwansasu Akifundisha somo la Njia ni Yesu katika kanisa la TAG sahara Spiritual Center.Waumini wakifuatilia neno kwa makini,
Imeelezwa kuwa njia
peekee ya kufikia mafanikio na uzima wa milele ni kumkubali Bwana Yesu kama
Bwana na Mwokozi wa maisha yako kama mwanadamu maana nyakati za leo kuna
matukio na njia nyingi.
Hayo yamesemwa na
mwinjilisti Kambona mwansasu wakati akifundiso somo la Yesu ndiye njia ile
katika kanisa la TAG Sahara Spiritual Center jijini Da es salaam.
Aidha mwinjilisti Mwansasu
alisema kuwa kuna njia nyingi ambazo mwanadamu anaweza kutumia kufanikiwa na
njia ni muhimu ili kufikia malengo ama jambo fulani,ila kupata na kufikia uzima
wa milele ni Yesu pekee hakuna mwingine.
Alisema kuwa hapo
awali katika bustani ya Edeni alikulaa matunda ya mti wa ujuzi wa mema na
mabaya na ndipo Mungu alimfukuza katika bustani na kuweka walinzi kulinda
bustani,Akifafanua alisema kuwa lengo la malaika hao waliokuwa wakilinda
bustani nia ni kulinda njia ya kurudi bustanini Adamu asije akala tunda la
uzima wa milele.
Hapo njia ndiyo
iliyofungwa na mpaka hapo Yesu alikuja na kuzaliwa kama mwanadamu kwa lengo la
kumkomboa mwanadamu ili uwepo na ushirika kati ya Mungu na mwanadamu,jambo
ambalo linawasaidia na kuwakomboa wanadamu katika madhaifu na magonjwa yao.
Akinukuu kitabu cha Yohana
14:6, 6 Yesu akamwambia,
Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.
7 Kama mngalinijua mimi, mngalimjua na Baba; tangu sasa mnamjua, tena mmemwona.
NA Yohana 5:24.
7 Kama mngalinijua mimi, mngalimjua na Baba; tangu sasa mnamjua, tena mmemwona.
NA Yohana 5:24.
24 Amin, amin,
nawaambia, Yeye alisikiaye neno langu na kumwamini yeye aliyenipeleka yuna
uzima wa milele; wala haingii hukumuni, bali amepita kutoka mautini kuingia
uzimani.
”Hakuna sababu ya kutumia njia zingine zaidi ya Yesu Pekee maana utakuwa na uhakika wa kufika kwake Baba wa Mbinguni,
Fanya bidii katika kumtafuta Yesu maana ndiye atakekuongoza kufika mbinguni ndiye njia sahihi wala wewe usikosoe wala lkuirekebisha.
Maana unakuta mwingine anaambiwa kuvuta sigara ni dhambi anaanza mjadala kuwa imeandikwa wapi? sasa pale utakapofahamu njia ya kweli kuwa ni Yesu hakuna sababu ya malumbano maan tayari unaifahamu njia."alisema mwinjilisti Mwansasu
”Hakuna sababu ya kutumia njia zingine zaidi ya Yesu Pekee maana utakuwa na uhakika wa kufika kwake Baba wa Mbinguni,
Fanya bidii katika kumtafuta Yesu maana ndiye atakekuongoza kufika mbinguni ndiye njia sahihi wala wewe usikosoe wala lkuirekebisha.
Maana unakuta mwingine anaambiwa kuvuta sigara ni dhambi anaanza mjadala kuwa imeandikwa wapi? sasa pale utakapofahamu njia ya kweli kuwa ni Yesu hakuna sababu ya malumbano maan tayari unaifahamu njia."alisema mwinjilisti Mwansasu
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni