YESU NI JIBU

Jumanne, 11 Novemba 2014

IFAHAMU BIBLIA YAKO: 8 OCTOBER 2014

1.  Kwa nini mfalme suleimani alipewa adhabu na Mungu wakati alianza vizuri naye kama mfalme wa Israeli?
Answer: kwa sababu ya kuabudu miungu ama kufuata miungu.
1wafalme 11:4(kukengeuka)mfalme alioa wanawake waliokuwa wanaabudu miungu mingi (1wafalme 11:5-8)
2.  Musa alikuwa mlimani na Mungu kwa muda usiopungua siku 80 ama miezi miwili na siku ishirini alikuwa akifanya nini
Answer:alikuwa akiandika amri kuu kumi za Mungu.
3.  kutokana na hilo ni nini kilichosababisha kukaa muda huu wote huko mlimani?
Answer:Ni kwa sababu awamu ya kwanza wana wa israeli waliasi na kuanza kuabudu sanamu ya ndama walioitengeneza na kusema ndiyo Mungu wao ndipo musa aliposhuka kutoka mlimani akavunja zile mbao mbili alizoandika amri,(kumbukumbu la torati 9:16,18)
Awamu ya pili siku zingine 40 Mungu alipomwita tena musa mlimani kwenda kumkabidi tena mbao mbili za mawe mfano wa zile za kwanza(kutoka 34:4)   
4.  Kwa muda wa miaka mitatu na nusu ambapo mvua haikunyesha juu ya nchi kwa neno la nabii Eliya yeye akiwa nabii alikuwa analishwa na nani? kwa muda huo wote.
Answer:kwa muda huo alijikuta akilishwa na kunguru na baadaye na mwanamke mjane wa sarepta(1wafalme 17:1-16) 
5.  Neno Familia kwa mtazamo wa kibiblia lina maana gani?Toa Sababu kama ama maana tano.
Answer:
·       Mume na mke waliooana hata kama hawana watoto.
·       Watu wa familia moja lakini vizazi tofauti tofauti.
·       watu wanaokaa nyumba moja hata kama ni kutoka ukoo tofauti tofauti(kutoka 12:3)
·       Watu waliofunga maagano ya kushirikiana kwa karibu;kama vile biashara,ndoa,mikopo,ardhi,utaifa,ndiyo maaana biblia inasema usifungiwe nira na wasioamini 2kor 6:14)
·       Watu wa kabila moja kama vile watoto 12 wa Yakobo walipofanyika vyanzo vya kabila 12 za Israeli(mwanzo 49:1,2,28).
SHIRIKI KUJIFUNZA BIBLIA NA KAMA UNAMONI TOA KWA NAMBA 0779632616 AU 0682672828.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni