YESU NI JIBU

Ijumaa, 28 Novemba 2014

NENO LA MUNGU BADO LINAHUBIRIWA PAMOJA NA KUWEPO KWA IMANI MBALIMBALI AMBAZO ZINAMASHAKA BADO WAHUBIRI WANAENDELEA KUTANGAZA NENO LA MUNGU KWA UFASAHA:

Serikali imetakiwa kuweka mikakati maalum ya kuwanusuru vijana wanaotumia na kusafirisha madawa ya  kulevya kwa lengo la kuwajenga vijana hao kuwa  wazalendo na kulitumikia taifa lao kwani baadhi ya yao wamekuwa wakipoteza maisha na wengine wameadhirika.
       Mchungaji Aidan Mabuka
Kauli hiyo imetolewa na mchungaji kiongozi wa kanisa la eagt mlima wa faraja mchungaji Aidan Mabuka katika mahojiano maalum na wapo redio katika mkutano wa injili ambao umeandaliwa na kanisa hilo lilopo yombo kisiwani kata ya sandali wilaya ya temeke jijini ambapo amesema kuwa ni vyema serikali ikaweka mikakati kabambe ya kuwanusuru vijana na kuwashirikisha viongozi wa dini.
Aidha amesema kuwa ni wajibu wa serikali na viongozi wa dini kuungana kwa pamoja kwa lengo la kuwasaidia na kuwanusuru vijana katika wimbi la utumiaji na uuzaji wa madawa ambao kwa sasa umekamata kasi katika baadhi ya mataifa na kuwapelekea vijana kuteseka na nguvu kazi ya taifa inapotea.
 Mhungaji kiongozi Mabuka akiwa na mke wake na wazee wa kanisa.
 Mke wa mchungaji Mabuka akifanya maombi kabla ya mchungaji kusimama kuhubiri katika mkutano wa injili ambao unaendelea katika viwanja vya Yombo kisiwani kwa fundi umeme jijini Dar es salaam.




Waimbaji mbalimbali wakihudumu katika mkutano huo wa injili ambayo mchungaji Aidan Mabuka ndiye mhubiri ambapo watu wengi wamefunguliwa na kuwekwa huru na wengi wamepokea uponyaji.
Watendakazi wa kanisa la mlima wa faraja EAGT wakiwa katika kuangalia kwa makini katika mkutano wa injili.





Watu waliofika katika mkutano wa injili kusikiliza neno la Mungu.
"Ni vyema kuwa karibu na vijana ambao tayari wamekata tamaa kwa lengo la kuwajenga upya kisaikolojia ili waweze kuwa na matumaini tena maana wengi wameshaona kuwa haiwezekani tena na hiyo mdiyo njia pekee kwa kuwaonesha upendo wa kristo nao wataweza kurudi,"alisema mchungaji mabuka.
Serikali kuu na ya mitaa inabidi iweke mkakati maalum wa kuwanusuru wananchi wake hasa vijana ambao wanateseke na kuwapelekea kushawishika kujiingiza katika makundi ya kihalifu hivyo ni wajibu wa serikali kubuni mbinu mbalimbali za kuwasaidia ikishirikisha viongozi mbalimbali wa dini.
Pamoja na hayo mchungaji mabuga hakuwa nyuma kutoa wito kwa viongozi wenzake wa dini kuacha kulumbana na kusemana vibaya badala yake ni kusaidiana ,kushauriana na kuombeana kwani ili waweze kumudu kupigana na adui ni sharti uwepo umoja na muungano ndipo wataweza  kupambana na adui.
Watumishi wa mungu ni vyema kuungana kwa pamoja ili kuwafikia vijana na jamii yetu inayotuzunguka ili wampokee yesu kama bwana na mwokozi wa maisha yao na kuachana na makundi mbalimbali ambayo hayasaidii wala haijengi mwili wa kristo.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni