YESU NI JIBU

Jumamosi, 4 Januari 2014

MOTO WA INJILI WAWASHWA NA MCHUNGAJI MTARAJIWA MASANJA MKANDAMIZAJI.

Mchungaji mtarajiwa awasha moto wa Injili katika viwanja vya serikali ya Mtaa Tabata Savana ambapo watu wengi walijitokeza kumpokea bwana YESU kama BWANA NA MWOKOZI wa maisha yao.
Kiukweli watu wengi wanapitia katika mapito magumu sana,akizungumza wakati wa kuhubiri mchungaji mtarajiwa Emanuel Mgaya maaru kwa jina la Masanja mkandamizaji ambaye pi ni mwigizaji wa komedi alisema kuwa MUNGU yupo tayari kuwasaidia qanadamu pale ambapo wameamua kujitoa kwake na kufuata maagizo yake kama alivyoagiza wanadamu kumtii yeye.
"Akinukuu kitabucha Yohana 5:5-11 alisema kulikuwa na mtu aliyekuwa mgonjwa kwa muda wa mika 38 kila wakati akitaka kuingia kwenye birika inapotibuliwa na malaika anashindwa kutokana na kutojiweza na ndugu zake wamwemwacha bila msaada wowote na YESU alimuuliza unataka nikufanyie nini? yeye kwa sababu ni mgonjwa anaanza kuta maelezo wakate angetakiwa kujibu nataka kupona,ndivyo ilivyo misha ya wengi sasa wanapitia katika mapito na magumu wanaanza kulalamika na kunung'unika"alisema mchungaji Mgaya.



Mtangazaji wa WAPO redio na pia ni mwimbaji wa nyimbo za injili Sila Mbise kushoto akiwa Masanja Mkandamizaji katikati na kulia nia mtume Peter Nyaga wakihojiwa katika studio inayotembea ya WAPO redio (OB VAN) katika viwanja vya Savana Tabata.
Mtume Peter Nyaga kulia akiwa na mchungaji mtarajiwa Emanuel Mgaya (Masanja Mkandamizaji).


 Mwimbaji Silas Mbise akiwajibika jukwaani.




Emanuel Mgaya mchungaji mtarajiwa akihubiri katika viwanja vya savana. 








Umati wa watu maelfu wakiwa wamekusanyika katika viwanja vya serikali ya mtaa wa Savana wakifuatilia kwa makini mahubiri na wengine wakiombewa katika viwanja hivyo.

Mwimbaji Ibrahimu Sanga awakiwajibika na vijana wake jukwaani.
NeemaJekoni hakuwa nyuma ya jukwaa wakati wa kuhudumu naye alipamba mkutano wa wimbo wake maarufu TUNAYE MWENYE UWEZO

Chezea Neema Gaspal wakati akiangusha kibao cha NI SHUJAA ambacho kwa sasa kinatamba katika redio mbalimbali za dini.

Neema GAspal kulia akiwa na Tumaini Njole wakiwa jukwaani kwenye mkutano wa injili savana.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni