Kutana na askofu mkuu wa WAPO mission International uweze kufahamu kwa undani juu falsafa ya umilikishaji kwa mujibu wa biblia
nikutambulishe rasmi kuhusu kampeni mpya ambayo WAPO MISSION INTERNATIONAL imeitangaza mwaka huu inayoitwa OPERESHENI MILIKISHA. Hoja ya leo ni kuitambulisha kwako kampeni hii kuanzia sababu zake, malengo yake na matarajio yake nini:
Propaganda za
kulinda amani
na kufuta
umaskini wa kipato
Amini usiamini, humu duniani kuna
mambo ya kustaajabisha ukiyagundua katika uhalisia wake. Naomba nitumie mfano hai wa vita vya wenyewe
kwa wenyewe vinavyoendelea Sudani ya Kusini. Mpaka ninapoandika makala haya; wakati
vita vinaendelea kwenye uwanja wa mapambano, na raia wasio na hatia wanauawa na
wengine kukimbia na kuyaacha makazi yao; eti vikao vya kutafuta amani nchini
humo vinaendelea jijini Adis Ababa Ethiopia, na pande mbili husika
zinajadiliana jinsi ya kusitisha vita!!
Swali la msingi ambalo haliko kwenye mjadala wa AdisAbaba ni Nani
anadhamini vita hivyo? Nani anayefanya biashara ya silaha zinazotumika kuuana
nchini Sudani? Je naye yuko kwenye kikao cha kujadili ajenda ya kusitisha vita
Sudani?
Ndivyo ilivyo na Vita dhidi ya
Umaskini wa kipato katika jamii za nchi zenye majina rasmi ya nchi za ulimwengu
wa tatu. Wakati rasirimali za asili (ambazo zina uwezo wa kufuta 100% umaskini
wa kipato wan chi husika) zinaendelea kuchukiliwa bure, au kwa manunuzi yasiyo
na tija kwa nchi husika; na kisha rasirimali hizo hizo zinazalisha bidhaa ambazo hurejeshwa
kwenye soko la nchi maskini kwa bei za
juu; na kutenegeza faida kubwa; eti matajiri wa ulimwengu wa kwanza
wanasadikiwa kudhamini mipango ya kufuta umaskini wa kipato katika nchi hizo
hizo zinazoporwa utajiri wake wa asili!
Hivi kweli kuna nia ya dhati (kutoka
kwa matajiri wa ulimwengu wa kwanza), ya kufuta umaskini wa kipato kwa nchi
maskini? Hivi kama kweli matajiri hao wangelitaka kuufuta kweli umaskini
ingewachukua zaidi ya miaka ya 50 kukamilisha zoezi hilo?
Nadhani tumefika wakati muafaka wa
kutokumung’unya maneno. Amani na utulivu, na kufutwa kwa umaskini wa kipato
haviwezi kutoweka kwa juhudi za matajiri wa ulimwengu wa kwanza, wakati
biashara zao zimejengwa katika misingi ya biashara ya kutengeneza na kuuza
silaha, na kupora rasirimali za asili kwa nchi maskini. Mwenye kutaka kuamini
kwamba kuna siku umaskini wa kipato utatoweka kutoka kwa matajiri atambue
kwamba umaskini wake ndio unaowaneemesha matajiri hao.
Mwenye nia ya
dhati ya kuleta amani
na kufuta
umaskini ni Mungu peke yake.
Ni Mungu peke yake ndiye awezaye
kutuliza ghasia na kurejesha amani na utulivu katika jamii; na kisha ndiye
mwenye nia na uwezo kufuta umaskini wa kipato kwa maskini.
Kwanini nasema hivi? Majibu ya swali hili ndiyo hoja maalum katika
makala haya. Naomba nistafsiriwe kuwa naleta majibu mepesi kwa maswali magumu.
Naomba nitumie fursa hii kuthibitisha ukweli, uzito na ushahidi ni kwanini
nasema Mungu peke yake ndiye mwenye ufumbuzi wa changamoto nilizozitaja hapa
juu.
Maono asilia ya Mungu kuhusu binadamu
Kwa wale tunaoamini kwamba
binadamu ameumbwa na Mungu kama livyoandikwa katika Biblia, tunao ushahidi wa
kimaandiko kwamba maono ya Mungu kuhusu binadamu hayakuwa na nia ya kumfanya
binadamu kuwa fukara na maisha ya fujo na ghasia duniani.
Tukisoma maandiko kuhusu maono ya
Mungu juu ya binadamu tusoma kwamba: “Mungu
akasema na tumfanye mtu kwa mfano wetu; na kwa sura yetu; wakatawale…..”
(Mw.1:26)
Andiko hili linadhihirisha bayana
kusudi la Mungu kuhusu binadamu hata kabla hajamuumba. 1. Kuumbwa kiumbe
anayeshabihiana na Mungu kwa fikra, hisia na utashi; 2. Kuumbwa kiumbe
atakayemwakilisha Mungu katika utawala wa dunia na viumbe vyote vilivyomo.
Kutokana na Maono haya Mungu
aliyatimiza kwa kuwaumba binadamu wa kwanza, Mwanamume na mwanamke, kama
ilivyoandikwa: “Mungu akaumba mtu kwa
mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba mwanamume na mwanamke aliwaumba. Mungu
akawabarikia, Mungu akawaambia, zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na
kuitiisha; mkatawale…..” (Mw.1:27-28)
Kutokana na ushahidi wa kimaandiko
tuliyosoma hapa juu, tunathibitisha kwamba binadamu wa kwanza waliumbwa katika
hali ya utukufu wa Mungu, na wakamilikishwa kuitawala nchi na viumbe vyote
vilivyomo. Kwa maelezo mengine ni kwamba, haki na mamlaka ya kumiliki ni
ya kimaumbile. Hisia ya kumiliki ni sehemu ya maumbile ya kila binadamu.
Pasipo kujali binadamu yuko katika
mazingira ya aina gani hisia ya kumiliki imo ndani yake. Maswali mengi
yanayojitokeza ni kama huu ndio ukweli tena wa kimaumbile kwa kila binadamu,
kwanini basi hivi sasa kuna matabaka ya maskini na matajiri, watumwa na
mabwana, waajiri na wajiriwa? Majibu ya maswali haya yanatupeleka kwenye sehemu
ya pili ya falisafa ya umilikishaji.
Kuvunjika kwa mahusiano na kupoteza mamlaka
Baada ya binadamu wa kwanza kuumbwa, na kumilikishwa kama
Mungu alivyowakusudia, binadamu hao hao walifanya maamuzi mabaya ambayo
yaliwagharimu matokeo mabaya. Mungu alipowamilikisha aliwapa sheria ya kutokula
matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya, na akawaonya kwamba siku
watakapokiuka sheria hiyo, watavunja mahusiano na yeye, na pia watapoteza sio
mamlaka ya utwala peke yake, bali wasitisha na maisha ya umilele duniani.
Adamu na Eva walipokiuka sheria ya Mungu; ghafla wakajikuta
wamefarakana na Mungu kama livyoandikwa: “…kwa sababu wote wamefanya
dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu;..” (Rum.3:23)
Kwa bahati mbaya, uvunjwaji wa sheria ya Mungu ulifanywa na
binadamu wa kwanza wale wale ambao ndio walitakiwa kubaki mfano wa vizazi vya
binadamu vinavyofuatia. Biblia imeandikwa kwamba:“Kwa hiyo, kama kwa mtu
mmoja dhambi iliingia ulimwenguni, na kwa dhambi
hiyo mauti; na hivyo mauti ikawafikia watu wote kwa sababu wote wamefanya dhambi.” (Rum.5:12)
Kutokana na maandiko tunaona kwamba kwa kosa la binadamu
kuliathiri vizazi vyote vya binadamu waliofuata baada yao. Na athari
hazikuishia katika kupoteza utukufu wa Mungu, bali ulisababisha kunywang’anywa
ile mamlaka ya utawala. Lakini Mungu atukuzwe kwa sababu hakuridhika na athari
zilizomsibu binadamu bali aliandaa mpango maalum wa kumkomboa na kumrejesha
katika asili yake ya kwanza. Mpango huu tutaupitia katika makala yajayo.
Itaendelea wiki ijayo
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni