YESU NI JIBU

Ijumaa, 17 Januari 2014

JE HUU NI UNABII AMA NI KITU GANI, KUWALISHA WAUMINI NYASI NA KUTAPISHA?

Hivi ndivyo hali halisi katika huduma ya Rabboni ya huko Afrika ya kusini ambapo kwa taarifa yako waumini wake wanaambiwa kuwa wakati wa kufunga na kuomba,pesa zile ambazo utatumia kwa kunywa chai ,chakula cha mcha na cha jioni fanya  mahesabu na kuwapelekea watu wanaopita katika mapito magumu na kuwapa sio kupeleka kanisani ila wape wao wasio nacho.
Huduma hiyo inayongozwa na kiongozi wake anayefahamika kwa jina la Lesego Daniel imekuwa ya namna yake jambo ambalo linaweza kuwa la kushangaza sana katika imani.
Ila yeye alikinukuu kitabu cha Yohana 14:12-14 ambayo inazungumzia pale YESU alivyosema kuwa yeye aniaminiye mimi na kazi nizifanyazo mimi yeye naye atazifanya naam na kubwa kuliko hizo atafanya kwa kuwa mimi naenda kwa BABA.
Sasa ndugu msomaji wangu hofu yangu ni hapa kulisha waumini nyasi je huo ndio unabii ama ni nini? ndiyo matendo ya kinabii au ndiyo matendo mkuu.





Hayo ndiyo yanayoendelea ndani ya huduma ya Rabboni center ministries ya huko Afrika ya kusini kazi kwako msomaji.






Mchungaji Lesego akitembea juu ya waumini wake



 Hapa zoezi la maombi na maombezi linaendelea mchungaji Lesego kupita juu ya waumini kwa kuwakanyaga.









Zoezi la kuaanza kutapika ndiyo unaoendelea kwa sasa




unaweza kutembela facebook ya kanisa hilo la Rabboni center ministries uli uweze kufahamu zaidi kinachoendelea katika huduma hiyo kwa sasa mwenye macho haambiwi tazama.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni