YESU NI JIBU

Jumamosi, 21 Desemba 2013

KONGAMANO LA VIJANA WENYE UMRI KUANZIA MIAKA 12 HADI 35 LAFANA SANA

Kongamano la vijana la kuridhisha maadili na uchumi endelevu likuwa la kufana sana kwani vijana wengi wamehudhuria na waimbaji mbalimbali nao wamehudhuria na kutoa burudani kwa vijana walioshiriki katika kongamano hilo.
Kongamano hilo limefanyika katika ukumbi wa BCIC Mbezi Beach jijini Dar es salaam ambapo walishiriki pia waalimu mbalimbali kutoa elimu na pia baadhi ya viongozi wa serikali nao walihudhuria katika kongamano hilo.
Vijana wengi waliohudhuria ni kuanzia miaka 12 hadi 35 na wengi wamekuwa na msisimuko mkubwa wa kutaka kufahamu hali halisi na jinsi ya kuweza kuridhi na zaidi ni kufahamu vipawa vyao katika jamii.
Kiukweli hili lilionesha jinsi vijana wengi walivyo na shauku ya kutaka kufahamu ni jinsi ganiwanaweza kuepukana na wimbi la umaskini na ukosefu wa kazi ama ajira.




Mwalimu Wilbroad Prosper akifundisha juu ya vipaji katika kongamano vijana ambalo limefanyika katika ukumbi wa BCIC Mbezi beach jijini Dar es salaam. 

 Askofu Slvester  Gamanywa akifundisha vijana kwenye kongamano


  askofu Gamanywa akimtambulisha mwanaharakati Renatus Mkinga.
 Mr Mkinga mara baada ya kutambulishwa na Askofu Gamanywa kwa vijana kwenye kongamano naye aliweza kuzugumza nao na kusema amefurahi kukutana na mwalimu wake wa chuo kikuu Profesa  Bavu.


Mkurugenzi wa idara ya michezo vijana na utamaduni akizungumza kwenye kongamano.








Mwimbaji wa Rapu ndugu Rungu la Yesu ambaye anatamba na kibao cha YESU okoa mitaa akiwa anatumbuiza katika ukumbu wa BCIC














 Hawa ni baadhi ya vijana waliohudhuria katika kongamano la vijana la kuridhisha vipawa na utajiri wakifuatilia kwa makini kongamano hilo.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni