Mapanga
yatumika kulinda Kanisa alipozikwa Ask.Kulola,
Miaka mitatu na siku 50 hivi, tangu Askofu Mkuu na
Mwanzilishi wa kanisa la Evangelistic Assemblies of God Tanzania (EAGT) DK.
Moses Kulola kumaliza kazi hapa duniani, (kufariki) hali si shwari ndani ya
kansia aliloacha, baada ya Makamu Askofu Mkuu, John Maene kufukuzwa katika
uongozi na uchungaji katika kanisa la Bungando, Mwanza, lilipo kaburi la
mwanainjili huyo na kuzua kiza kinene katika mustakabali wa kiroho.
Habari za ndani toka ndani ya kanisa hilo zinaeleza kuwa
tangu kutwaliwa kwa kiongozi huyo, ilizuka hali ya sintofahamu kwa kile
kilichodaiwa kuwa ni kutoelewana baina ya wale wanaoelezwa kuwa ni “wa Kulola”
yaani wafuasi wake sugu na wale wa
kizazi kipya kinachotaka kubadili mambo na kujenga himaya mpya.
Ni katika hali hiyo, hivi karibuni aliyekuwa Makamu Askofu
Mkuu wa Kanisa hilo, John Maene, alifukuzwa uongozi na uchungaji kwa kile
kilichodaiwa kuwa alipatikana na tuhuma za ukiukaji wa kimaadili, lakini
akapinga tuhuma mbele ya Halmashauri ya kanisa na kasha kufungua Kesi katika
mahakama Kuu kanda ya Mwanza.
Taarifa zilizothibitishwa na mmoja wa wazee wa kanisa la
Buganda (Jina linahifadhiwa kwa sasa) zinaeleza kuwa, kiongozi huyo alifungua
shauri la Madai Mahakama kuu mwanzoni mwa wiki iliyopita, sambamba na kuomba
amri ya mahakama ya kuzuia utekelezaji wa maamuzi ya Halmashauri ya kanisa wa
kumfukuza hadi pale shauri ilililopo mahakamani litakapopata ufumbuzi.
“Tayari tumepata amri ya Mahakama, lakini pia vijana
wameamua kulilinda kanisa kutokana na njiama zinazoendelea chini kwa chini
kwani wachungaji wanaotaka kutekeleza amri “haramu” wamejifungia kwenye kanisa
moja wakiendelea kujadiliana hatujua wanapanga nini,”alisema Mzee huyo ambaye
alisema wazi kuwa wanasimama na kiongozi wao (Askofu Maene) hadi dakika za
mwisho na kuwa Mungu atawatetea.
MTIRIRIKO WA MATUKIO
Mtiririko wa matukio yanayoashiria kuwa hali si shwari ndani
ya kanisa la EAGT, yalianza wiki
iliyopita baada ya kikao cha Halmashauri kuu na Baraza la waangalizi wa kanisa
hilo, vilivyofanyikia mjini Dodoma kuamua kuizinisha kutimuliwa kwa Makamu
Askofu Mkuu kwa kile kilichodaiwa kuwa alituhumiwa kukiuka maadili.
Hata hivyo, Makamu huyo alipopewa nafasi ya kujitetea mbele
ya Baraza la waangalizi alikanusha tuhuma hizo ambazo inadaiwa kuwa chanzo
chake ni unabii uliotolewa na mmoja wa manabii wa kanisa hilo, na wajumbe
wakaonekana kumuelewa, lakini uongozi wa kamati kuu ukatishia kujiudhulu na
kuliacha kanisa ikiwa wajumbe wangekataa kuidhinisha mpango huo, ndipo maamuzi
yakafikiwa.
Miongoni mwa waliohudhuria kikao hicho ni Mjane wa Marehemu
Askofu Kulola Elizabeth Kulola, ambaye hakukubaliana na wenzake baada ya
kumuuliza mtuhumiwa akakanusha tuhuma zake.
WAZEE WAFUKUZWA BUGANDO
Nyakati linafahamu kuwa baada ya mambo kwenda mrama, Makamu
Askofu Maene, aliondoka mjini Dodoma na kurejea Mwanza ambapo Jumamosi baadhi
ya wazee wa kanisa walimtaka aende kwenye kikao kujadili suala la kufukuzwa
lakini, hakwenda aliwajibu kuwa wangekutana ibadani na Jumapili asubuhi alienda
ibadani kama vile hakuna kilichotokea, lakini alipopanda madhabahuni baada ya
nyimbo za sifa, kuabudu kumalizika alieleza mkasa wote na kueleza msimamo wake
kuwa yeye bado ni Makamu Askofu Mkuu wa EAGT, mpaka suala la kile
anachotuhumiwa litakapojadiliwa na Mkutano Mkuu.
Kasha aliwaeleza waumini kuwa yeye ni mchungaji kiongozi wa
kanisa hilo kihalali na kasha akawatimu wazee wa kanisa ambao walituhumiwa kuwa
wachochezi. Majina ya wazee tunayahifadhi mpaka tutakapowapa nafasi ya
kujitetea) .
Baada ya msimamo huo kanisa lilirindima kwa shangwe na
kuahidi kumuungamkono mchungaji wao hadi tone la mwisho la mapambano
waliyoyaita ya kutetea haki yao,
WACHUNGAJI WATIMUA MBIO
Baada ya tukio la Jumapili mapambano yalihamia mahakamani
ambapo jumatatu wanasheria walitinga Mahakama Kuu na kufungua shauri, lakini
Jumatano mambo yalibadilika baada ya kuwepo kwa tetesi kuwa barua ya kumtimua mhungaji
wao ilikuwa mikononi mwa wajumbe wakiipeleka
na kuwa mchungaji mbadala kutoka shinyanga alikuwa tayari amefika mwanza
mjini.
Waumini wakakumbushana kuwa huenda amri ya mahakama isingeheshimiwa
kama ilivyotokea Jijini Dar es Salaam, ambapo mahakama ya Wilaya ya Temeke
ilitoa amri ya kuzuia mkutano wa kanda uliokuwa umeitishwa kwa dharura na amri
ya mahakama ikafikishwa kwa wadhamini, lakini wakaendelea na kasha wakatekeleza
uamuzi waliokusudia kuufanya.
Ni katika hofu hiyo inaelezwa kuwa vijana shupavu wa kanisa
la EAGT Bugando, wakayanoa mapanga na kujaa katika viwaja vya kanisa huku
wakisisiza kuwa wako tayari kwa lolote
ili kumlindaz mchungaji wao.
Majira ya saa tatu asubuhi Mjane wa Askofu Kulola alifika
kanisani hapo na kwenda moja kwa moja kwenye kaburi alipozikwa mumewe Akaka juu
yake na kuwasema kuwa yote yatokee
lakini mtu asisogelee kaburi hilo.
Inaelezwa kuwa maneno hayo yalizidisha ghadhabu ya walizni
na wakati ikisubiriwa nini kitatokea, baadhi ya wachungaji wanaominika
kuungamkono maamuzi ya kanisa walifika kanisani hapo lakini wakakumbana na
vitisho vya vijana hao ambapo walilazimika kutimua mbio, huku wengine wakiruka
ukuta kujiokoa. (majina ya wachungaji
walionusurika tunayahifadhi kwa sasa).
Nyakati ilipompigia Katibu Mkuu wa EAGT, Mch.Leonald Mwezarubi,
simu yake iliita tu bila kupokelewa kwa muda mrefu.
Askofu Mkuu
wa EAGT, Dr.Brown Mwakipesile alipoulizwa kuhusu hali hiyo na
mtakabali wa kanisa alisema kwa kifupi kuwa kanisa linaandaa tamko na kwa sasa
wana lakusema.
Tangu
alipofariki Askofu Mkuu na mwanzilishi wa kanisa la EAGT Dr.Moses
kulola, Agosti 29, mwaka 2013 katika hospitali ya AMI (African Medical
Investments) iliyopo Slipway jijini Dar es Salaam, alipokuwa amelazwa baada ya
kurejea kutoka katika matibabu huko
India kumekuwa na mfululizo wa matukio yanye utata yaliyoanza hata kabla ya mwiliwake kurejeshwa mavumbini.
Tukio la kwanza lilikuwa lile la bodi ya wadhamini wa kanisa la
Tanzania Assemblies of God (TAG) kwenda mahakamani kuwasilisha pingamizi la
kutoruhusu mwili wa Dkt. Moses Kulola kuzikwa katika viwanja vya kanisa hilo
lililopo maeneo ya Bugando jijini Mwanza wakidai ni mali yao.
Lakini sasa wamerejea tena mahakama
ile ile na safari hii ni makamu askofu anayelalamika kuonewa na kukiukwa kwa
kanuni kikatiba na utawala wa haki
katika kumsimamisha uongozi na kumvua uchungaji.
NGUVU ZA ASKOFU MAHENE
Ingawa wengi wanautazama mgogoro huo
kama unaomhusu mtu mmoja lakini ukweli ni kuwa nyuma ya Mchungaji Mahene ambaye
ni mzee wa miaka 70 hivi kuna umati wa wachungaji kutoka kanda ya ziwa
waliomuwezesha kuwa na upinzani mkali
katika uchaguzi wa viongozxi wa kanisa hilo mwaka jana.
Nyakati linafahamu kuwa katika
uchaguzi huo, Mhane, Mwezarubi na mwakipesile walikuwa na ushindanbi katika
nafasi ya Askofu Mkuu na kusababisha kura kurejewa mara tatu, hadi pale
Mwezarubi alipoamua kujitoa na kusalia, Mwakipesile na Mahene.
Ni katika marudio hayo, Mwakipesile
aliibuka mshindi na baadaye mshindani wake (Mahene) akatwaa nafasi ya makamu
Askofu na Mwezarubi akawa katibu mkuu, hivyo watatu hawa wana nguvu
zinbazokaribiana ndanbi ya kanisa hilo.
HOFU
YA KUGAWANYIKA KWA EAGT
Wakati
sasa makabiliano yakihamia kortini kuna kila dalili za kanisa hilo ambalo mwanzo
wake ni kugawanyika kutoka TAG, likagawanyika tena kufuatia kile kinachoelezwa
kuwa ni hofu ya kuandamwa kwa wale wanaoitwa “wa-Kulola” yaani wanasalia
kushika misingi aliyoacha mzee wa Injili Kulola na wanahofiwa kuwa tishio
katika siasa za kanisa.
Mmoja
wa wachungaji waliopo karibu na uongozi aliliambia nyakati kuwa kinachoendelea
sasa ni kulisafisha kanisa kwa mambo mawili maombi na kufuata kanuni kwa kuwaondoa wale
wanaoonekana sio watii na waliotenda dhambi.
“Tuko
kwenye maombi tunamuomba Mungu mtu akileta ujanja na uwezo wake atapambana na
Mungu, mkuu amesema anasafisha kanisa hata wakibaki nane wanaoshika imani hao
watatosha vinginevyo atajiondoa akafanye kazi zingine…”alisema mmoja wa
wachungaji waliopo karibu na uongozi wa sasa.
Aidha
imeelezwa kuwa kufuatia hali hiyo ya “Matengenezo” baadhi ya waqchungaji
wamekuwa na hofu kwa kile kinachoelezwa kuwa “mwenzio akinyolewa tia kichwa
maji” hali inayompa Askofu Mahene nguvu ya kusaidiwa.
TETESI
ZA BUGANDO KUREJEA TAG
Wakati
tukienda mitamboni kulienea madai kuwa mgogoro wa EAGT, Bugando unaweza
kutimiza usemi kuwa “Vita vya panzi ni karabu ya mjusi” kwani kanisa hilo kwa
muda mrefu lilikuwa na mvutano baina ya EAGT na TAG, na nyaraka yaani hati za
ofa wanazo TAG, hivyo itakuwa vigumu kwa uongozi wa EAGT kulitetea ipasavyo
kortini.
Ni
hali hiyo inayoleta wasi wasi kuwa mambo yakienda vibaya linaweza kujikuta
likirejea mikononi mwa TAG, lakini hakuna msemaji yeyote baina ya makanisa hayo mawili
aliyekuwa tayari kuzungumzia tetesi hizo.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni