kutoka kushoto ni mkuu wa idara ya elimu masafa katika taasisi ya elimu ya watu wazima wakiwa na mkurugenzi wa Brothers Academy katikati na kulia ni makamu mkuu wa shule ya hiyo Kelvin Oguta wakiwa katika mahafali.
Mkuu wa idara ya Elimu mmasafa Taasisi ya watu wazima ndugu Baraka Kionywaki akizungumza katika mahafali ya ASSA katika shule ya Brothers Academy iliyopo Banana jijini Dar es salaam.
Mkurugenzi wa BROFOA akizungumza katika mahafali ya ASSA katika shule hiyo iliyoko Banana jijini Dar es salaam
Mkurugenzi wa Brothers Academy akimlisha keki mmoja wa wanafunzi wa ASSA katika shule ya Brothers Academy
Vijana wa Brothers Academy wa Adventist secondary student association ASSA wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kukabidhiwa vyeti.
Na Stelius
Sane,
Wanaomiliki
vituo vya kutolea elimu isiyo katika mfumo rasmi wameaswa kusajili vituo hivyo
kwa lengo la kutoa elimu bora na kutambuliwa na serikali maana kuendesha
shughuli ya kutoa elimu bila kusajiliwa na serikali ni kinyume cha sheria.
Kauli hiyo
imetolewa na mkuu wa idara ya elimu masafa taasisi ya elimu ya watu wazima
ndugu Baraka Kionywaki wakati akizungumza katika mahafali ya Adventist
secondary student association iliyofanyika katika shule ya Brothers academy
iliyoko Banana jijini Dar es salaam.
Akizungumza
katika mahafali hayo amesema kuwa kazi kubwa ya shule na vituo vinavtyotoa
elimu ya sekondati ya miaka miwili katika mfumo usio rasmi ni toa elimu kwa
akushirikiana na serikali katika jitihada ya
kutoa elimu huria kwa watanzania .
Aidha
aliongeza kuwa serikali ilitoa maagizo mwaka 2013 ya kusajiliwa kwa vituo vyote
vinavyotoa elimu ya mfumo usio rasmi ili kupatiwa namba ya usajili na taasisi
ya elimu ya watu wazima ndiyo iliyo pewa mamlaka ya kufuatilia ubora wa elimu
inayotolewa na vituo hivyo na kutokana na hilo kituo cha brothers Academy
ilimepewa usajili wa kutoa elimu kwa jamii katika mfumo usio rasmi yaani
Qualified Test(QT).
Alisisitiza
kuwa ni vyema vituo vyote vinavyotoa elimu katika mfumo huo visajiliwe na
kutambuliwa na serikali ili kuweza kutoa
elimu ili serikali ikague na kuruhusu kutumika maana elimu inayotakiwa kutolewa
kwa watanzania kuwa ni elimu bora.
Kwa upande
wa shule ama kituo cha brothers Academy ndugu Kionywaki alisema kuwa ni moja ya
shule ambayo imesajiliwa chini ya elimu ya watu wazima na imekuwa ikifanya
vizuri katika vituo vilivyotambulika na serikali kutokana na kuwa na walimu
waliopata elimu ya juu kutoka katika
vyuo vikuu vya ualimu vinatambuliwa na serikali.
"Brothers
Academy ni moja ya shule ambayo imefanya vizuri katika mitihani ya maarifa na
katika mkoa wa Dar es salaamu imekuwa ni shule ya kwanza na katika shule bora
tano Tanzania zinazotoa elimu katika mfumo usio rasmi ni mojawapo hivyo
inafanya vizuri sana",aliema ndugu Kionywaki.
Hata hivyo alitoa
wito kwa wadau wote wanaotoa elimu katika mfumo usio rasmi nchi nzima kufuata
utaratibu ambayo umetolewa na serikali wa usajili ili kutoa elimu bila tatizo
lolote maana serikali inaunga mkono mfumo wa utoaji wa elimu katika mfumo huo.
Na amesema
kuwa ikiwa wadau hao watashindwa kufuata taratibu ambazo zimewekwa na serikali
basi sheria itafuata mkondo wake maana elimu inatakiwa elimu bora kwa
watanzania na sio bora elimu kwa sababu ya tamaa ya fedha.
Naye mzee wa
kanis la waadvetisti Mzee Kasaja amesema kuwa maadaili ndiyo njia pekee
inayosaidia mwanafunzi kufanya vizuri pale aatakapoamua kufuata na kuachana na
njia ambazo hazimpendezi Mungu.
Aliongeza
kuwa wadau wa elimu wanaotoa elimu kwa jamii katika mfumo usio rasmi kwa ujumla
inasaidia kupunguza uhalifu mitaani maana vijana wengi watakuwa
wanajishugulisha na masuala ya kupata elimu tofauti na kukaa bure mtaani.
Kwa upande
wa mkurugenzi wa shule ya Brothers Academy ndugu Robart Rwezaura alisema kuwa
wanaendesha huduma ya kutoa elimu katima mfumo usio rasmi,elimu huria kwa lengo
la kuhakikisha kuwa watanzania wanapata elimu bora itakayowasaidia kufanya
vizuri katika maisha yao.
Alisisitiza
kuwa chanzo cha mafanikio kwa kila mwanafunzi anayesoma hapo Brothers ni kumcha
na kumtanguliza Mungu katika maisha yao na ndiyo maana wamewaruhusu wanafunzi
kumtafuta Mungu katika maisha yao ya kila siku.
Ndugu
Rwezaura ameongeza kuwa wao hapo kituoni wanawalimu waliohitimi katika vyuo
vinavyotambuliwa na serikali na hao wanawasaidia wanafunzi kwa kuwafundisha na
pia hiyo inachangia sana wanafunzi kufanya vizuri katika mitihani yao.
Hata hivyo
hakuwa nyuma kuelezea suala la maadili katika shule yao kuwa kwa asilimia kubwa
mwanafunzi akiwa namaadili mema ni rahisi kusaidika na kuelekezeka na njia hiyo
kuwasaidia kufikia malengo yao ya kupata elimu bora.
Shule ya Brothers Academy inapatikana
maeneo ya Banana jijini Dar es salam
kw amawasiliano ya namba 0717280669, 076780669
na 078780669
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni