YESU NI JIBU

Ijumaa, 29 Julai 2016

JIMBO LA TEMEKE LIMEONYWA KUWA MAKINI NA MGOGORO UNAOENDELEA AMBAO TAYARI UPO UMEFIKISHWA MAHAKAMANI:

Mwenyekiti wa Bodi ya wadhamini wa kansia la EAGT, Mzee Henri Mfuko, ameonya kuwa kansia hilo linakabiliwa na hatari ya kugawanyika kufuatia mgogoro ulioibuka baina ya uongozi wa kanda na ule wa Jimbo la temeke ambao umesababisha kufunguliwa kwa kesi ya madai mahakamani na kusimamishwa kwa viongozi wa Jimbo. Huku ikielezwa kuwa kivuli cha Hayati Askofu Dk. Moses Kulola ndicho kinacholityesa kanisa hilo.
Aidha imeelezwa kuwa  Wothia alioandika kulola Kabla ya kufariki dunia unaompa Katunzi kijititi cha kuhubiri Injili, kukua kwa kasi kwa kansia la EAGT City Centre na mpango wa kujenga majengo ya kisasa ya Jimbo la Temeke viliibua upinzani mkubwa  uliopelekea kuvuliwa  madaraka  na kugawanywa kwa Jimbo bila kufuata taratibu.
Ni kwa sababu hiyo, Askofu Katunzi na wenzake waliamua kufungua shauri la madai Mahakamani na ikatolewa amri ya kuzuia mkutano lakini  haikuheshimiwa na badala yake  mkutano ukafanyika na viongozi wa muda wakateuliwa.

Kwa mujibu wa vyanzo vyetu ndani ya kanisa hilo, lililomiongoni mwa makanisa makubwa ya kipentekoste Tanzania, hali ya kutofautiana baina ya Uongozi wa kanda chini ya Askofu Nicodemus Nyenye na kamati yake, na uongozi wa Jimbo la Temeke chini ya Askofu Floriana Josepah  Katunzi na Kamati yake  umeshindwa kupata ufumbuzi  na kupelekea kufunguliwa kwa  shauri la madai namba  70 ya mwaka 2016,  katika mahakama ya Wilaya ya Temeke.
Habari kutoka mahakamani hapo zinaeleza kuwa  Kesi hiyo ilifunguliwa na Askofu Katunzi na wenzake, dhidi ya Bodi ya wadhamini  ya kanisa la EAGT, Jumatatu iliyopita ambapo pia waliomba amri ya mahakama ya kuzuia mkutano wa dharura  ulioitishwa na uongozi wa kanda  bila kutaja agenda zake.
Pamoja na amri hiyo ya mahakama kikao hicho kiliendelea kama kilivyopangwa na kikafanya mambo mawili ambayo ni kuligawa Jimbo la Temeke na kuzaliwa Jimbo la Ilala na kutangazwa kwa viongozi wa muda wa Jimbo la Temeke naada ya uongozi wa kanda kusimamisha kamati iliyoongozwa na Askofu Katunzi.
Katibu wa Kanda ya Mashariki na Kusini ya kanisa la EAGT, Mch. Dk. Alphonce
Mwanjala, akiongea mbele ya wajumbe wa mkutano huo wa dharura alisema kuwa maono yao (kanda) sio kujenga bali ni kuhubiri Injili, lakini Jimbo la Temeke maono yao ni kujenga.
Alisema kuwa uongozi imewasimamisha viongozi hao na kuteua  vionmgozi wa muda kwa kuwa waliwaita Askofu Katunzi  mara tatu, lakini hawakufika hivyo hawana njia nyingine isipokuwa kuweka kando.
Baada ya kauli hiyo hali  ilichafuka kumbuni baada ya baadhi ya wachungaji kupaza sauti zao kupinga hatua hiyo hadharani wakisema kuwa inauonevu na harufu ya hofu kutokana na kasi ya maendeleo ya Jimbo na mpango wao wa kujenga jengo la ofisi za lenye ghorofa tatu.
Mmoja wa wachungaji aliyekuwa akilia machozi alisema: “Hiki ni kivuli cha Askofu Dk. Kulola kinachoendelea kulitesa kansia letu. Tumekuwa na mpango wa maendeleo  ya jimbo ikiwa ni pamoja na ujenzi wa jingo la ghorofa tatu  na michoro ilishakabidhiwa kanda na hilo ndilo limewafanya wagawe Jimbo ili kutudhoofisha. Unajua Kanisa letu la EAGT halina ofisi rasmi, Kanda haina ofisi n ahata makao makuu ni jina tu, hatua ya sisi kupeleka mchoro wa Jengo la Ghrofa tatu ndio chanzo cha yote haya…..”alisema Mchungaji huyo ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini.

MSIMAMO WA MDHAMINI
Akiongelea mgogoro huo, Mwenyekiti wa Bodi ya wadhamini wa kansia la EAGT, Mzee John Henri Mfuko, alisema kuwa kwa hali ilivyo kanisa hilo linakabiliwa na hatari kubwa ya kugawanyika vipande viwili kwa kuwa kuna baadhi ya viongozi wanaofanya mambo kinyume na katiba tena kwa kutofuata utaratibu.

Mdhamini huyo alisema kuwa mgogoro uliopo baina ya Jimbo la Temeke na Kanda ya Mashariki usingefika mahali ulipo sasa kama katiba ya kanisa ingelifuatwa na viongozi kushughulikia matatizo kabla ya kukua na kuwa migogoro mikubwa.
Alitoa mfano wa mgogoro uliotokea huko Shinyanga ambapo yeye alikwenda na kusimamia suluhu ambayo hatimaye ilipatikana na pande mbili kumaliza tofauti zao.
“Kuna kiongozi wa kanda alikuwa hapa juzi nikamwambia haya mambo si mgeyamaliza tu kwanini mfikia hatua ya kuondoana? Akanisambia huyo jamaa amemtukana kiongozi wetu siwezi kumacha lazima aondolewe tu,”alisema mzee huyo huku akiinamisha kichwa kuonyesha ishara ya kuumizwa na mgogoro huo.
 wameusimamisha uongozi wa Jimbo la Temeke kwa kuwa  ulipinga kugawana.
Wakati uongozi wa kanda ukidai kuwa uongozi wa Jimbo uliitwa mara tatu ili kusaka suluhu na kisha  kutohudhuria, madai ya Uongozi wa Jimbo kulingana na barua  waliyomuandikia Askofu Mkuu wa Kanisa hilo wakikata rufaa kupinga tatibu zilizotumika kugawa  Jimbo hilo ni kuwa, utaratibu wa kawaida wa kugawa Jimbo haukufuatwa kwa kuitishwa kwa halimashauri ya jimbo kujadili  kabla ya mpango kufikishwa kanda.
Uongozi wa Jimbo pia katika malalamiko yake kwa Askofu Mkuu walitaka awasikilize yeye kwa kuwa hawakuwa na Imani na uongozi wa kanda, hata hivyo uongozi wa taifa uliandika barua na kurejesha shauri hilo ngazi ya kanda ambayo jimbo haikuwa na Imani nayo katika kushughulikia mgogoro huo.
Habari za ndani zinadai kuwa kumekuwa na njama mbaya za kumzushia Katunzi kashfa ili kumvua cheti cha uchungaji  na kuleta hofu miongoni mwa wachungaji wa Jimbo la Temeke ambao hawakubaliani na hatua ya kumvua uongozi.
Wengi wa wachungajin wa Jimbo hilo walisema wazi kuwa hawako tayari kukubaliana na maamuzi hayo kwa kuwa hawakupewa nafasi ya kusikia pande zote n ahata kulipigia kura jambo hilo.
KIVULI CHA KULOLA
Habari za ndani zionaeleza kuwa  baada ya Askofu  Kulola kumaliza kazi, ulisomwa wosia alioandika kuhusu familia yake   ambao ulimtaja Katunzi kuwa  msimamizi wa mirathi ambapo pia alitajwa kukabiziwa kijiti cha kuhubiri injili katika ziara ambazo kiongozi huyo alikuwa akizifanya.

Ni kutokana na kile kinachoelezwa kuwa ni hofu ya kile kilichoandikwa katika wothia huo, mambo kadhaa yametokea ikiwa ni pamoja na baadhi ya wanadugu wa Dk. Kulola kupinga Katunzi asisimamie mirathi  ya kulola na hata alipochaguliwa  kuwa Askofu wa Jimbo la Temeke kivuli cha yale yaliyoandikwa katika wothia kiliendelea kumwandama.
Kanisa la EAGT, lilianzishwa  baada ya kutoke mgogoro  baina ya Dk. Kulola, na Immanuel Lazaro waliokuwa vionmgozi wa juu wa kansia la TAG, Lazaro akiwa Askofu Mkuu na Kulola akiwa makamu wake.
Inaelezwa kuwa mgogoro mkubwa ulianzia katika kuhamisha wachungaji na uliposhindwa kusuluhishwa ndani ya kansia  na kufikia hatu ya kupigana ulifikishwa  mahakamani  na mahakama iliamua kila mmoja afanyekazi kivyake na wagawane mali.

Ni kutokana na hitoria hiyo hofu ya kumeguka tena kwa kanisa la EAGT imejitokeza  miongoni mwa waumini n ahata mdhamini pia.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni