YESU NI JIBU

Jumatano, 2 Mei 2012

Chanzo cha nguvu ya Mungu na uwepo wa Roho mtakatifu ndani ya kanisa ni pale tu kanisa ulimwengu walipojitoa katika kushirikiana na taifa la Israeli.

Kauli hiyo imetolewa na Askofu mkuu wa huduma ya maombi na ushauri wa kibiblia (BCIC) na pia ni msimamisi mkuu wa WAPO MISSION INTERNATIONAl Askofu Silverster Gamanywa katika mkesha uliofanyika katika kanisa hilo siku ya ijumaa ya tarehe 27 april.

Amesema hayo wakati akielezea lengo la ziara ya kuwaongoza waumini mbalimbali katika safari ya kutembelea taifa la Israel ambapo ziara hiyo itakuwa mwezi wa saba mwaka huu.

Baraka za Mungu zimetoweka katika mataifa mengi kutokana na waumini kutoshirikiana na taifa la Israeli  kusema kuwa kuna baraka za Mungu ambazo bado zinaandamana na wana wa Israeli likiwepo baraka ya kubariki taifa hilo nawe utabarikiwa na ukilaani taifa hilo utalaaniwa.

Kwa mkiristo halisi lazima aunganishwe na baraka za taifa hilo maana ni makosa kutengana na taifa hilo maana ukienda kinyume nawe wewe ni adui wa taifa hilo

Aidha Askofu Gamanywa amesema kuwa umaskini wa taifa la Tanzania limetokana na kutokuwepo kwa muunganiko na taifa hilo

Akielezea juu ya gharama za kuchangia ni dola za kimarekani elfu mbinu na mia tisa ambayo ni gharama ya tiketi ya ndege,hoteli ,chakula pamoja na nauli za usafiri za ndani wakati wote wa ziara.

Hata hivyo ameongeza kuwa ataongoza maombi na maombezi katika taifa hilo na kuahidi kuwa endapo watu watakubali kutembelea taifa la Israeli watakuwa wameungana na baraka za baba wa imani Ibrahimu.

Njia ya kuweza kufanya ni kurejesha uhusiano na taifa  hilo pili utainuka kiuchumi maana hoteli utakazolala ni za taifa hilo na vyakula na usafiri utakaotumika ni ya waisraeli hivyo utakuwa umechangia katika pato la taifa hilo na kuunganishwa na baraka za taifa.







Hakuna maoni :

Chapisha Maoni