Watanzania
wametakiwa kuacha dhambi na kumgeukia Mungu kabla Mungu hajashusha
ghadhabu kali katika taifa.
Kauli hiyo
imetolewa na askofu wa kanisa la end time ministry askofu Frank
Kilavatitu wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es
salaam ambapo amesema Mungu amemtumwa kuwaambai watanzania watubu
dhambi na kuziacha zao.
Askofu
Kilavatitu amesema kuwa katika maono yake Mungu amesema amechukizwa
na uovu wa Tanzania ambao umekidhiri na watanzania wasipotubu
ghadhabu itafuatia ambayo ni maji ya mvua yatakayosababisha maafa
makubwa kwa muda wa siku saba.
Akifafanua juu
ya dhambi na uovu ambao umekidhiri juu ya taifa la Tanzania ni baadhi
ya viongozi wa dini kutoa kafara ya damu na wengine kujiunga na dini
ambazo zinakwenda kinyume na maadili za MunguAkifafanua juu ya dhambi
na
Hata hivyo
ameongeza kuwa baada ya siku saba za toba wakikaidi atapiga taifa kwa
maji kama ilivyotokea kwa siku za Nuhu na watu watdhani kuwa ni kiama
kumbe ni fimbo ya Mungu kwa watanzania.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni