YESU NI JIBU

Jumanne, 28 Februari 2023

ZITAMBUE GHARAMA AMBAZO UTAGHARAMIKIA UKIMWAMINI BWANA YESU.

Askofu Zakaria Osward Rude akimwongoza sala ya toba kijana ambaye alifika kanisani hapo na kuamuua kumwamini bwana Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yake.

 Imebainishwa kuwa kila mwamini anatakiwa kutambua kuwa kuna gharama za kulipa ukimwamini Yesu katika maisha ya kila mwamini ambaye amemkiri kwa kinywa chake kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yake.

Hayo yamebaibishwa na askofu Zakaria Oswald Rule wakati akifundisha neno la Mungu katika ibada ya jumapili katika kanisa la Jesus Save Fellowship lilopo Karakata jijini Dar es salaam.

Aidha amesema kuwa kumfuata Yesu kuna gharama ambazo ni lazima kila anayetaka kumwamini na kumfuata atalipa ndipo ataweza kuishi maisha ya kumpendeza.

"Yesu amesema Kila anayetaka kunifuata lazima aikane nafsi yake na ndipo achukue msalaba wake anifuate,huwezi kumfuata Yesu ukiwa na namna ya kutokuwa tayari kulipa hizo gharama".alisema askofu Rule.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni