YESU NI JIBU

Ijumaa, 17 Februari 2023

SERIKALI YAPONGEZWA NA WATETEZI UHAI

Mkurugenzi wa Shirika la Kimataifa la Kutetea Uhai la Human Life International (HLI) Kanda ya  Afrika kwa Nchi zinazozungumza kiingereza, Emil Hagamu amesema kupiga marufuku Vitabu vya Ziada Vinavyotoa mafundisho kinyume na Mila na desturi za Tanzania kuendane na kupiga marufuku chanzo kinacholeta vitabu hivyo.

Alisema pia marufuku hiyo iendane na kukomesha vitendea kazi vinavyowezesha Mapenzi ya jinsi moja na makundi yanayohamasisha matendo hayo maovu zikiwemo Diplomasia zinazohamasisha.

Akizungumza kufuatia hatua hiyo Hagamu ameipongeza Serikali kwa hatua iliyochukua ya kupiga marufuku vitabu 16 ambavyo maudhui yake yanakwenda kinyume na mila, desturi na tamaduni za Tanzania.

Alisema WAZIRI  wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda, akitangaza uamuzi huo mbele ya waandishi wa habari alisema shule yeyote itakayobainika kuwa na vitabu hivyo hatua kali zitachukuliwa dhidi yake ikiwemo kufuti wa usajili wa shule husika.

“Vitabu hivyo havipaswi kutumika shuleni na kwenye taasisi za elimu kwa kuwa vinakinzana na mila, desturi na utamaduni wa mtanzania”. Alisisistiza Prof.Mkenda

Alivitaja vitabu hivyo kuwa ni diary of a wimpy kid, diary of a wimpy kid-Rodrick rules, diary of a wimpy kid-the last straw, diary of a wimpy kid-dog days, diary of a wimpy kid-the ugly truth, diary of wimpy kid-cabin fever, diary of a wimpy kid-the third wheel, diary of a wimpy kid-hard luck.

Vingine ni diary of a wimpy kid-the long haul, diary of wimpy kid-old school, diary of a wimpy kid-double down, diary of wimpy kid-the gateway, diary of wimpy kid-diper overlode, Is for transgender(you know best who you are), Is for LGBTQIA(Lesbian, gay, bisexual, transgender, queer/questioning(one’s sexual or gender identity) intersex, and asexual/ aromantic/ agender; kwa jinsi mbili kukutana na kuleta ongezeko la Watu" Alisema Hagamu.

Aidha Hagamu pia alivitaka Vyombo vya Habari kukataa, kutangaza habari zilizoko kinyume na desturi, Mila za Watanzania;

that make you you na sex education a guide to life.

Kwa mujibu wa Hagamu licha ya kwamba hatua ya kupigwa marufu Vitabu hivyo.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni