Rais Magufuli ametuma salamu za
rambirambi kwa familia na wote walioguswa na kifo cha aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa
Manyara Dr Joel Nkaya Bendera kilichotokea jioni ya leo katika Hospitali ya
Taifa ya Muhimbili alipokuwa anapatiwa matibabu.
Rais ameeleza kuwa amesema marehemu
atakumbukwa kwa mchango wake mkubwa alioutoa kwa Taifa akiwa kiongozi katika
nyadhifa mbalimbali zikiwemo Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Naibu Waziri na Mbunge na
pia kwa mchango wake mkubwa katika maendeleo ya michezo.
“Dkt. Joel Nkaya Bendera alikuwa
kiongozi shupavu, mahiri na mchapakazi, alipenda kufanya kazi kwa ushirikiano
na daima alitamani kupata mafanikio makubwa katika majukumu aliyokuwa nayo,
hakika tutamkumbuka” – Rais John Magufuli
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni