Luka 16:19-31" akasema,palikuwa na mtu
mmoja,tajiri,aliyevaa nguo za rangi ya zambarau na kitani safi,na kula siku
zote kwa anasa.na maskini mmoja jina lake lazaro,huwekwa mlangoni pake,ana
vidonda vingi,naye alikuwa akitamani kushibishwa kwa makombo yaliyoanguka ktk
meza ya yule tajiri;hata mbwa wakaja wakamlamba vidonda vyake.
Ikawa yule
maskini alikufa,akachukuliwa mpaka kifuani kwa ibrahimu.yule tajiri naye akafa
akazikwa.basi,kule kuzimu akayai ua macho yake,alipokuwa ktk mateso,akamwona
ibrahim kwa mbali,na lazaro kifuani mwake.akalia,akasema,ee baba
ibrahimu,nihurumie,umtume lazaro achovye ncha ya kidole chake
majini,auburudishe ulimi wangu;kwa sababu ninateswa ktk moto
huu.
Ibrahimu,akasema,mwanangu,kumbuka ya kwamba wewe uliyapokea mambo mema yako ktk maisha yako na lazaro
vivyo alipata mabaya;na sasa yeye yupo hapa anafarijiwa,na wewe unaumizwa.na
zaidi ya hayo,kati yetu sisi na ninyi kumewekwa shimo kubwa ili wale watakao
kutoka huku kwenda kwenu wasiweze;wala watu wa kwenu wasivuke kuja
kwetu.akasema,basi baba nakuomba umtume kwenda nyumbani kwa baba yangu,kwa kuwa
ninao ndugu watano,ili awashuhudie,wasije wao pia wakafika mahali hapa pa
mateso.ibrahimu akasema,wanao musa na manabii;na wawasikilize
wao.akasema,la,baba ibrahimu,lakini kama akiwaendea mtu atokaye kwa
wafu,watatubu.akamwambia,wasipowasikia musa na manabii,hawatawashawishwa hat
mtu akifufuka ktk wafu"
habari hii inamtaja tajiri na lazaro,Tajiri ni
muumini ndani ya kanisa.
luka 16:22-25kawa yule maskini alikufa, akachukuliwa na malaika mpaka kifuani kwa
Ibrahimu. Yule tajiri naye akafa, akazikwa.Basi, kule kuzimu aliyainua macho
yake, alipokuwa katika mateso, akamwona Ibrahimu kwa mbali, na Lazaro kifuani
mwake. Akalia, akasema, Ee baba Ibrahimu, nihurumie, umtume Lazaro
achovye ncha ya kidole chake majini, auburudishe ulimi wangu; kwa sababu
ninateswa katika moto huu. Ibrahimu akasema, Mwanangu, kumbuka ya kwamba wewe uliyapokea
mambo mema yako katika maisha yako, na Lazaro vivyo alipata mabaya; na sasa
yeye yupo hapa anafarijiwa, na wewe unaumizwa.
tajiri anamuita ibrahimu baba,hivyo ni muamini
sawa na kitabu cha wagalatia 3:7" fahamu basi,ya kuwa wale walio wa
imani,hao ndio wana wa ibrahimu "
MUNGU anakuona wewe ni tajiri.
ufunuo 2:9" naijua dhiki yako na umaskini
wako,(lakini u tajiri)najua na matukano ya hao wasemao ya kuwa ni wayahudi,na
sio,bali ni sinagogi la shetani"
*biblia inasema yule tajiri alikila kwa anasa.
*kula neno la mungu pasipo kutumika hiyo ni anasa.
"kufutahia tu mahubiri pasipo kuyatendea kazi
ni anasa.
*kupoteza wakati na kuwa na udhuru mwingi ni
anasa.
*kutojitoa kwa ajili ya bwana ni anasa.
##tunapaswa kujichunguza##
*lazaro ni mchungaji.
*amewekwa mlangoni ili akuchunge uwe salama.
*yohana 10:9" mimi ndimi mlango,mtu akiingia
kwa mimi,ataokoka,ataingia na kutoka,naye atapata malisho"
*mchungaji huutoa uhai wake kwa ajili yako.
*yohana 10:11" mimi ndimi mchungaji
mwema.mchungaji mwema huutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo"
*adui ajapo kukushambulia wewe kwanza humuanza
mchungaji ili usiwe salama.
*marko 14:27" yesu akawaambia mtakunguwazwa
ninyi nyote kwa ajili yangu usiku huu;kwa kuwa imeandikwa,nitampiga mchungaji
na kondoo watatawanyika"
*bw.yesu alisema wazi kuwa kanuni ya adui ni
kimshambulia mchungaji kwanza ndipo amfikie kondoo.
*tajiri(muumini)alimlisha lazaro (mchungaji) makombo.
**je!mchungaji wako anakula makombo?
**yohana 4:34"yesu akawaambia,chakula changu
ndicho hiki,niyatende mapenzi yake aliyenipeleka,nikaimalize kazi yake"
**mchungaji anahitaji kazi ya mungu isonge
mbele.ndiyo chakula chake.
*pasipo kazi ya mungu kusonga mbele hupata
vidonda.
"ponya vidonda vyake visije kulambwa na mbwa.
*vidonda vya mchungaji hupona pale aonapo ujenzi
ndani ya kanisa unakamilika.
*vidonda hupona mchungaji aonapo watu wanaokoka.
*vidonda vya mchungaji hupona aonapo watu
wanaongezeka kiidadi kanisani na wanakua kiroho.
**nini unafanya kwa ajili ya mchungaji
wako?unamlisha makombo?
*unapoponya vidonda vya mchungaji wako
utajihakikishia usalama wako na uzao wako.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni