ASKOFU wa kanda ya kati kanisa la Pentecostal Holliness Association Mission (PHAM) Julias Bundala amewataka waumini wa madhehebu ya dini kuhakikisha kuwa wanatumia fursa zinazojitokeza kwa wakati huu ambapo serikali imeamua kuhamishia makao yake makuu mkoani Dodoma.
Kiongozi huyo wa kanisa hilo ametoa ushauri huo wakati alipokuwa akizungumza na watumishi mbalimbali wakiwemo wachungaji,wainjilisti,wazee wa kanisa na mashemasi kwenye semina ya siku nne iliyoandaliwa na kanda ya kati iliyofanyika kijiji cha Chiwe wilaya ya Kongwa mkoani Dodoma.
Amesema kuwa kutokana na uamuzi wa serikali kuhamishia makao yake ya nchi mkoni humo ni wakati sasa kwa waumini kuelekeza nguvu zao kwenye fursa zinzojitokeza ili waweze kujiinua kimapato na kuondokana na umasikini.
Akizungumza kwa upande wa viongozi wa kanisa hilo wakiwemo wachungaji,wainjilisti,wazee wa kanisa na mashemasi,aliwataka kuwa na ubunifu wa miradi itakayowaongezea kipato ili waweze kuondokana na changamoto walizonazo kwenye maisha yao ya kila siku ikiwemo ya kiroho na kimwili.
Aliwataka viongozi hao walioshiriki katika semina hiyo iliyowashirikisha kutoka makanisa ya kanda hiyo ya kati ,askofu huyo amewataka kuwa na maono ya ubunifu katika utumishi wao yatakayowasaidia kuleta mapato ya kiuchumi kwa ajili ya maisha yao na jamii inayowazunguka.a kila siku.
Amesema na ili waweze kukamilisha katika utumishi wao huo wanatakiwa kuwa vielelezo katika nafasi zao kwa uwajibikaji kwa kuonyesha matendo yao kwa uwazi ili wanaowatumikia wawezi kujifunza kutoka kwao.
Pia askofu huyo alilitaka kanisa hilo kuhakikisha wanatumia muda wao mwingi kuiombeaserikali pamoja na viongozi wa nfgazi mbalimbali ili waweze kuifanya kazi zao kwa ueledi na hofu ya kimungu.
Aidha katika maombi hayo pia amewataka viongozi hao kuelekeze kwenye kumwaombea rais aweze kutimiza yale yote ambayo yaliyo kuwa magumu kutekelezeka katika vipindi vilivyopita vya viongozi waliomtangulia ili afanikishe ndani ya uongozi wake wa awamu ya tano.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni