Wazazi wanatakiwa kuwa makini na watoto wao hasa wale ambao
wanapenda kuwapeleka watoto shule za kulala (boarding)iwe ya wasichana
wenyewe ama ya wavulana wenyewe,ni
vizuri kuwa makini na kuhakikisha kuwa kila unapompeleka shuleni akirudi hakikisha
kuwa unamsikiliza na kukaa naye ili ufahamu kuwa amekutana na changamoto gani
akiwa huko shuleni.
Wazazi wenzangu nimekaa na kutafakari sana juu ya watoto
wanaopelekwa shule za kulala watoto maana hali ni mbaya katika shule hizo
maarufu kama (boarding).
Unaweza kulauliza ni kwanini nasema hivyo je sipendi watoto
wasome shule za (boarding) hapana napenda tena sana ila sasa kilanachotokea ni
kwamba watoto hao wanakutana na changamoto mbalimbali na wanajifunza na kuiga
tabia ambazo ni mbaya na zinapelekea hata kushindwa kufanya vizuri katika
masomo yao.
Watoto wengi wanaosoma katika shule za kulala hasa wasichana
pekee yao wanafundishana kufanya mapenzi ya jinsia moja sasa mtoto anarudi likizo hata mzazi hana muda wa kukaa naye
wala kuzungumza naye mpaka tena shule inafunguliwa anarudi mzazi,mlezi
hujafahamu changamoton na yale yanayomsimu mtoto.
Kwa upande wa shule za kulala watoto wa kiume nayo
changamoto ipo kama ya wasichana nao
wanafanya na kufundishana mapenzi ya jinsia moja(ushoga) unakutana na kijana
mtaani anajihusisha na masuala hayo unaanza kujiuliza umeanza lini,wapi? kumbe
mzazi wewe ndiye uliyefungua mlango.
Unaweza kusema kuwa mimi mwanangu anasoma shule
inayoendeshwa kwa misingi ya dini,swali Je unauhakika kuwa mwanao anajifunza
dini ama anasikiliza wakati wewe hujamfundisha na hujawahi kuzungumza naye? ni
swala la kujiuliza na kuwa makini nayo la sivyo utakuwa unaandaa kizazi
kitakachokuwa shida.
Mzazi inakupasa kuwa makini na watoto ambao Mungu amekupa
uwalinde uwasaidie wamjue na kumtambua Mungu wa kweli katika maisha yao,maana
inakuwaje mzazi mwanao anarudi kutoka shuleni hata siku moja hujawaki wakupa
muda wa kuzungumz anaye mapaka anarudi shuleni,
kibaya zaidi mzazi unakuwa nyumbani mwanao wa kiume anamleta
rafiki wake wa kike anakaanaye nymbani kwako chumba kimoja baba mama hujui hilo
si tayari ni tatizo halafu unasema kuwa wewe ni mzazi ama mlezi utakuwa
unamatatizo hapo ghorofani (nikiwa na maana kichwani mwako)huwezi kuwa baba
mama ama mlezi kwa namna hiyo wewe ni bora mzazi na sio mzazi bora,narudia wewe
ni bora mzazi na sio mzazi bora.
Pamoja na maisha kuwa magumu na kukimbizana kila kukicha ni
vyema ukatenga muda wa kuzungumza na watoto wako hata kwa dakika tano
tafakari maana ndiyo sababu Mungu kakuamini na kukupa nafasi hiyo ya kuwa
baba,mama au mlezi.
Watoto wengi wanapokuwepo mashuleni hujifunza mambo mengi
ambayo hata mzazi unaweza kushangaa na kuchanganyikiwa usimuliwa yale mwanao
anafanya,wengine wanafundishwa uchawi na ushirikina,usagaji,ushoga,wizi,ujambazi,matumizi
ya madawa ya kulevya na mengine mengi yafananayo na hayo,mzazi upo wapi?
Kiukweli mimi binafsi inaniumiza kuona mzazi huna nafasi ya
kukaa na watoto wako eti unadai wewe ni mkurugenzi,mhandisi,mchungaji,askofu,shekhe,Imamu
na hata vyeo vyote ambavyo wewe unaweza kujiita,familia yako(watoto)ni wa
muhimu kwanza kuliko hayo mengine.
Leo niishie hapa ila tujifunze kukaa na kuzungumza na watoto
wetu waonyeshe upendo wa dhati na usiwanyime fimbo kama biblia inavyosema katika
kitabu mithali 23:13-14 ambapo imeandikwa kuwa Usimnyime mtoto wako
mapigo;Maana ukimpiga kwa fimbo hatakufa.Utampiga kwa fimbo,na kumwokoa nafsi
yake na kuzimu.
Kwa maswali ama jambo lolote nisms ama piga 0625620902 au
0779632616
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni