Bi Sofia Abrahamu akliombewa na mchungaji Katunzi jumapili iliyopita baada ya kufika madhabahuni kutoa sadaka ya shukrani na kutengua mafungo na nguvu za mizimu ambayo imekuwa ikimwandama
Bibi ambaye hakufahamika jina lake mara moja akishuhudia jinsi Mungu alivyomponya wakati aliteseka kwa muda mrefu bila mafanikio ila baada ya maombezi Mungu alimponya nasasa ni mzima anatembea bila Gongo.
Bibi ambaye hakufahamika jina lake mara moja akiwa na mchungaji Katunzi ambaye alikuwa na shida kwenye mguu hali iyopelekea kutafuta msaada katika njia mbalimbali na kulekea kuambiwa afanyiwe upasuaji iliyogharimu milioni 9 na Baada ya maombi na maombezi alianza kutembea hali iyopelekea kumtukuza Mungu na kutembea bila kushika tena gongo ambapo hapo awali alikuwa hawezi.
Waumini waliofika kanisani hapo EAGT City Center wakifuatilia neno kwa makini ambalo mtumishi wa Mungu mchungaji Katunzi alifunzisha hayupo pichani.
mchungaji Florian Katunzi Akiwaombea waumini waliofika madhabahuni kuombewa wakati wa kuhitimisha kongamano la maombi la siku tatu ndani ya kanisa la EAGT City Centter wiki iliyopita
Mchungaji Katunzi akionesha fimbo ya kutembelea ambaye alikuwa akitumia mwanamke aliyefika kanisani hapo kutafuta maombi na maombezi na baada ya maombezi alitembea huku washirika wakishangilia matendo mak
Mwanamke ambaye amefahamika kwa jina la SOfia Abraham akishuhudia matendo makuu ambayo Mungu amemtendea ndani ya kanisa la EAGT City center
Wahudumu wakiwasaidia watu waliodondoka wakati wa maombi na maombezi kwa watu waliofungwa na nguvu za giza mizimu ya ukoo na shida mbalimbali.
Kongamano la siku tatu ndani ya kanisa la eagt
city center limekuwa msaada kubwa kwa baadhi ya watu ambao walikuwa wanteseka
kwa muda mrefu ssan katika maisha ya o hali iliyopelekea kushindwa kustawishwa
katika maisha yao.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti watu mbalimbali
waliofika katika kanisa la EAGT City Center waliokuwa na matatizo mbalimbali
wasimulia walivyokutana na Jemedari Yesu na kuwafunguwa na kuwaweka huru katika
maisha yao.
Mwanamke ambaye amefahamika kwa jina la bi sofia abrahamu
mwasumbi alisema kuwa kupitia kongamano
la siku tatu la maombi alisema kuwa kwa muda mrefu amekuwa akiteseka katika
maisha yake.
Akizungumza mbele ya kanisa hilo alisemea kuwa kwa
muda mrefu amekuwa akipoteza fedha na kutesemka katika maisha yake kila
anachokifanya hakifanikiwi n a amekuwa akipoteza fedha kwa muda mrefu hali
ambayo imesababisha maisha yake kushindwa kufanikiwa .
“Nimeteseka sana katika maisha yangu maana katika
familia yetu watnafamilia huwa akifa anafariki kutokana na ugonywa wa
kuapararalize kupooza,ugonjwa ambayo inawattesa familia na kwa sasa name
ninapata gansi upande wa kushoto”,alisema bibi Sofia.
Kutokana na hilo niliamua kujiunga na kanisa la
EAGT CITY CENTER ambapo kulikuwa kuna maombi ya ukombozi na kufunguliwa
yaliyokuwa yakiongozwa na mchungaji Florian Josephat Katunzi na Mungu
alinitendea muujiza nimefunguliwa na kuwekwa huru kwa sasa ni jambo la
kumshukuru sana Mungu.
“Tangu nianze kuwa mshirika wa kanisa hili Mungu
amenitendea mambo makuu sana nimepona na ninaendelea vizuri nimetengwa na
mateso na magonjwa ya kila namna na ninasimama kwa sasa mbele za Mungu na
madhabahu kutangaza ushindi wa Mungu katika maisha yangu”alisema Sofia
Akiwaongoza katika maombi na maombezi mchungaji Katunzi alinukuu kitabu cha Zaburi
107:13-14 Wakamlilia Bwana katika dhiki zao, Akawaponya na shida zao. Aliwatoa katika giza na uvuli wa
mauti, Akayavunja mafungo yao.ni wakati wako Mungu kukutoa katika mateso na
taabu za kila namna maana yeye ndiye kimbilio la wote wenye miili.
Mchungaji Katunzi aliongeza kuwa inawezekana umeteseka kwa
muda nrefu kiasi kwamba umekata tamaana kuona kuwa haiwezekani tena kama biblia
inavyosema kuwa akawaponya na shida zao leo Mungu kwa jina la Yesu Krisyto
anaachilia nguvu ya uponyaji na uzima
juu ya kila mmoja aliyeingia ndani ya kanisa hilo.
Aliongeza kuwa Mungu anamponya mtu ambaye
amejitenga na uovu na kusimama katika zamu yake na kuishi maisha ya utakatifu
pamoja na kuliitia jina la Yesu Ili ufunguliwe katika mateso mbalimbali na
magonjwa sawa na kitabu cha zaburi
103:3-5 inayosema kuwa Akusamehe maovu yako yote, Akuponya magonjwa
yako yote,Aukomboa uhai wako na kaburi, Akutia taji ya fadhili na
rehema,Aushibisha mema uzee wako, Ujana wako ukarejezwa kama tai;
Ni kwanini unakubali kuteseka na
kudanganywa na waganga wa kienyeji wakati Yesu mtenda miujiza Yupo kukuponya na
mateso na magonjwa mbalimbali yanayokusibu katika maisha yako inawezekana
hakuna kufanikiwa ndani ya familia,ukoo ana jamaa yako kutokana na mateso na
vifungo mbalimbali mliofungwa ni wakati wa kukataa na kusima katika zamu yako
ili bwana Yesu akufungue.
Kutokana na hilo mchungaji Katunzi
ameendelea kutoa mwaliko kwa wale wote wanaoonewa na kuteseka kutokana na nguvu
za giza,mizimu mafungo ya kila namna ili Mungu awafungue maana yeye Yupo tayari
kuwasaidia wanadamu na kuwaweka huru katika maisha yao ya kielimu,kiuchumi na
kiafnya.
Ndugu
msomaji fuatilia mafundisho ya mchungaji Florian Katunzi kipindi cha saa ya
ushindi na kufunguliwa kinachorushwa na Star TV kila siku ya jumamosi saa moja hadi saa mbili usiku na marudio ni
alhamisi saa nne na nusu hadi saa tano na nusu asubuhi.
Kwa
mawasiliano piga simu namba 0718261717,0784367826 au 0754367826
Au
tembelea www,pastorkatunzi.blogspot.com
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni