YESU NI JIBU

Alhamisi, 1 Desemba 2016

UZINDUZI WA TAASISI WA ASKOFU MATHAYO SULEIMAN ULIOFANYIKA JIJINI DAR ES SALAAM KWA LENGO LA KUWASAIDIA WENYE MAHITAJI MBALIMBALI

 Wa nne kutoka kushoto ni mwenyekiti wa Mathayo Suleiman Foundation mchungaji Eliasaph Mathayo  na kulia kwake ni naibu katibu mkuu wa wizara ya mambo ya ndani ya nchi balozi Simba Yahya wakiwa katika picha ya pamoja baada ya uzinduzi wa taasisi hiyo.



Na Stelius Sane,
Wadau wa maendeleo wameaswa kuwasaidia watu wasiojiweza katika maisha yao kuhakikisha kuwa wanafanikiwa na kuishi watu wengine wanavyoishi bila kujali dini kabila rangi wa utaifa wake.
Hili limetokea kwenye uzinduzi wa taasisi ya askofu Mathayo Suleman ambayo imezinduliwa na rasmi na naibu katibu mkuu wa wizara ya mambo ya ndani ya nchi balozi Simba Yahya jijini Dar es salaam.
Akizungumza katika uzinduzi huo Balozi Yahya alisema kuwa serikali inatoa huduma kwa jamii yote inawazunguka ila kutokana na nchi inayoendelea na uchumi wake ni mdogo amewasihi wadau mbalimbali  na taasisi za kibinafsi kujitokeza na kusaidia serikali kutoa huduma ambazo serikali pekee yake haiwezi.
Aidha Balozi Yahya alisema kuwa serikali inaangalia taasisi mbalimbali na asaszi za kijamii ambazo wanaweza kujiunga na kukusanya nguvu pamoja na kuwasaidia  wanachi kutatua changamoto mbalimbali zinazowakumba kama vile huduma za kiafya.
Akifafanua juu ya huduma za afya alisema kuwa serikali inashirikiana na asasi binafsi na tasisi za kidini kuwapa huduma wananchi wanaowazunguka na serikiali nayo inawaongezea nguvu ili kutatua changamoto za kiafya kwa wanachi wake.
Kwa upande wa mwenyekiti mtendaji wa Mathayo Suleiman Foundati Bwana Eliasaph Mathayo alisema kuwa taasisi hiyo inaungana na wanchama mbalimbali wa tasisi hiyo na kuchanga fedha na mahitaji mbalimbali kwa lengo la kuwasaidia wale wenye uhitaji.
Alisema kuwa taasisi hiyo inamalengo ya kuwasaidia watu wasiojiwezakwa kutoa fursa za mafunzo ya elimu ya ufundi stadi na ujasiriamalikwa makundi yenye shida ili yaweze kujitegemea katika maisha yao ya kila siku.
Bwana Mathayo aliongeza kuwa taasisi hiyo inampango wa kuanzisha vituo vituo vya afya vitakavyotoa huduma bora za afya sehemu zenye mapungufu pamoja na elimu ya uzazi na malezi ya mtoto pamoja na kuanzisha miradi ya kiuchumi kwa wanawake na vijana ili wawe na uhakika wa kupata mahitaji yao ya msingi ya maisha.
"Tuna lengo la kuanzisha vituo vya habari na usambazaji habari na kutoa misaa wa hali na mali kwa wafungwa na wakimbizi", alisema Bwana Mathayo wakati akizungumza na gazeti hili wakati wa uzinduzi wa taasisi hiyo.

Hata hivyo amesema wataendelea kuishi kwa kufikia malengo ya watu wasiojiweza ili kuhakikisha kuwa nao wanasaidika na kuishi katika maisha nzuri kama watu wengine wanavyoishi,na pia kuhakikisha kuwa wanawake na vijana wanawezeshwa ili kuinua hali zao kimaisha kwa kuwapa fursa za kujiendeleza kielimu na kupata huduma bora za afya.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni